• Maswali
  • Wasiliana Nasi
  • English

Jamhuri ya Muungano wa TanzaniaWakala wa Majengo Tanzania

  • kuhusu Sisi
    • Ujumbe kutoka kwa Mtendaji Mkuu
    • Sisi ni Nani
    • Dira na Dhamira
    • Tunafanya Nini
    • Mikakati
    • Mkataba wa Huduma
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Bodi ya Ushauri
    • Muundo wa Taasisi
    • Senior Management
    • Kurugenzi wa Uwezeshaji wa Huduma
    • Kurugenzi ya Ushauri
    • Kurugenzi ya Ujenzi
    • Kurugenzi ya Miliki
    • Meneja wa Mikoa
  • Nyumba
    • Nyumba za Kuuza
    • Nyumba za Kupangisha
    • Fomu ya Ununuzi wa Nyumba
    • Fomu ya ununuzi wa Nyumba
  • Miradi
    • Miradi Tunayoishikilia
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Iliyo Katika usanifu
    • Miradi Tunayotegemea kufanya
  • Machapisho
    • Machapisho
  • Kituo Cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha
  • Ununuzi
    • Mpango wa Manunuzi wa Mwaka
    • Mialiko ya zabuni
    • Orodha ya Wazabuni Walioshinda

Habari Mpya

  • PROF. MBARAWA AIPONGEZA TBA UFUNGUZI WA MAJENGO YA KISASA DAR ES SALAAM

    tokea siku 2
  • PAC YATEMBELEA MRADI WA TEMEKE KOTA

    tokea siku 3
  • KAMATI YA BUNGE YAITAKA WIZARA YA UJENZI KUISAIDIA TBA.

    tokea wiki 1
  • BODI YA USHAURI YA TBA YATEMBELEA MRADI WA UJENZI WA TEMEKE KOTA.

    tokea wiki 2

Latest Press Release

TBA YAADHIMISHA SIKU YA WANAWAKE DUNIANI.

Imewekwa: Thursday 09, March 2023

“Ubunifu na mabadiliko ya Teknolojia, chachu katika kuleta usawa wa kijinsia ni kauli mbiu iliyobeba maadhimisho ya siku ya wanawake duniani yaliyofikia kilele chake Machi 8, 2023. Maadhimisho hayo yaliambatana na maandamano yaliyofanyika katika mikoa mbalimbali nchini pamoja na maonesho ya bidhaa mbalimbali zilizotengenezwa na wanawake wajasiriamali.

Wafanyakazi wanawake wa Wakala wa Majengo Tanzania (TBA) waliungana na wanawake wengine dunia kusherehekea maadhimisho hayo ambayo yalifanyika katika mikoa mbalimbali nchini.

Viongozi mbalimbali walioudhuria sherehe hizo waliwapongeza wanawake na kuwataka waendelee kufanya kazi kwa bidii pamoja na kuendana na mahitaji ya teknolojia. Akizungumza wakati wa sherehe hizo katika viwanja vya Mnazi mmoja Mkuu wa mkoa wa Dar es Salaam Mhe. Amos Makalla ametoa ujumbe kwa wanawake wa mkoa wa Dar es Salaam kuwa Serikali ya Awamu ya sita inayoongozwa na Mhe. Rais Dkt. Samia Suluhu Hassan inatambua umuhimu wa mwanamke hivyo ni vyema wanawake wakatumia fursa zinazopatikana katika jamii kwa kufanya ubunifu unaoendana na teknolojia ya sasa.

Awali Mtendaji Mkuu wa TBA Arch. Daud Kondoro alitoa baraka zake kwa wanawake wa TBA kabla ya kuanza kwa maandamo hayo katika ofisi za Wakala jijini Dar es Salaam. Pia Arch. Kondoro aliwapongeza wanawake wa TBA kwa kazi nzuri wanazozifanya kila mmoja katika eneo lake ambazo zimekuwa chachu ya mafanikio ya Wakala na taifa kwa ujumla. "Kama kauli mbiu yenu inavyosema Ubunifu na mabadiliko ya Teknolojia, chachu katika kuleta usawa wa kijinsia hivyo kila mnachokifanya hapa TBA, kinaonekanakuwa na tija kwa maendeleo ya taasisi yetu" aliongeza Arch. Kondoro.

Wanawake wa TBA wamemshukuru Mtendaji Mkuu pamoja na menejimenti ya TBA kwa kuwawezesha kutekekeza majukumu yao katika maeneo mbalimbali.

Tanzania Census 2022

Mawasiliano yetu

TBA
THE CHIEF EXECUTIVE, TANZANIA BUILDINGS AGENCY (TBA), 13 MOROGORO ROAD, P.O BOX 94, 41102 VIWANDANI, DODOMA TANZANIA, EMAIL: ce@tba.go.tz Website: www.tba.go.tz
Nukushi :
Namba ya Simu : +255 733 483 437, +255 677 108 010
Barua Pepe : barua@tba.go.tz

Linki za Haraka

Linki Linganifu

  • WIZARA YA UJENZI NA UCHUKUZI
  • Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo
  • Utumishi
  • Tume ya Takwimu ya Taifa
  • Tume ya Ajira

©2023 wakala wa majengo tanzania . Haki zote zimehifadhiwa..

Imesanifiwa, Imetengenezwa na Mamlaka ya Serikali Mtandao.Inaendeshwa na Wakala ya Majengo Tanzania