i. Mratibu wa Miradi
ii. Mbunifu Majengo Mkuu,
iii. Mkadiriaji Majenzi Mkuu,
iv. Mhandisi Majengo Mkuu,
Majukumu Kitengo cha Uratibu wa Miradi.
Kitengo cha Uratibu wa Miradi kina jukumu la kuhakikisha upatikanaji wa taarifa za miradi inayosimamiwa na Wakala zinapatikana ili kuandaa na kuwasilisha taarifa zote za kisera. Aidha, kitengo pia kinafuatilia maendeleo ya miradi kupitia Timu za miradi ikiwemo ile inayosimamiwa na mikoa.
Aidha, Kitengo kimepewa jukumu la kuratibu shughuli zote zinazofanywa na Ofisi za Mameneja wa Wakala wa Mikoa yote ya Tanzania Bara.
Majukumu makuu ya kila Sehemu (section) ni kama ifuatavyo;
Sehemu ya Ubunifu Majengo, inalo jukumu la kufanya ubunifu Majengo mapya na yale ambayo yanahitaji ukarabati, pamoja na kusimamia ujenzi au ukarabati katika Majengo ya Wizara au Taasisi za Serikali.
Sehemu ya Uhandisi Majengo, hufanya Ubunifu wa Kihandisi wa Majengo na kusimamia ujenzi wa Majengo mapya na yale ambayo yanahitaji ukarabati. Pia kitengo hufanya ukaguzi wa miradi ili kubaini upungufu wa viwango katika Ubunifu wa Kihandisi na usimamizi wa Ujenzi, kwa miradi ya Serikali ambayo inashughulikiwa na washauri wengine.
Sehemu ya Ukadiriaji Majenzi inalo jukumu kuu la uandaaji wa makabrasha ya zabuni na ya utekelezaji wa ujenzi, vilevile Bajeti za miradi na ushauri kwenye udhibiti wa gharama za ujenzi.
Wajibu wa Idara ya Ushauri, Wakala wa Majengo Tanzania, ni kutoa Ushauri Elekezi kwa Wizara na Taasisi mbalimbali za Serikali katika fani zifuatazo;
i. Ubunifu Majengo
ii. Ukadiriaji majenzi
iii. Uhandisi Majengo
Huduma zinazotolewa ni;
i. Ushauri Elekezi katika hatua ya Upembuzi yakinifu,
ii. Ushauri Elekezi katika hatua ya Uandaaji wa michoro,
iii. Ushauri Elekezi katika hatua ya Uandaaji wa Makabrasha ya Zabuni na Mikataba,
iv. Ushauri Elekezi katika hatua ya utekelezaji wa Ujenzi au Ukarabati.
v. Usimamizi wa Shuguli za Ujenzi (Projects Management).