Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Mhe. Daniel Chongolo atembelea mradi wa ujenzi wa nyumba za makazi ya wananchi Magomeni kota uliosanifiwa na kujengwa na Wakala wa Majengo Tanzania (TBA) na kuridhishwa na kasi ya ujenzi wa mradi huo unaotarajiwa kukamilika mnamo mwezi Desemba mwaka huu.
Wakala wa Majengo Tanzania (TBA) unaandaa Mpango Mkakati mpya hii ni baada ya Mpango Mkakati wa awali kuisha muda wake.
Wakala wa Majengo Tanzania (TBA), imenunua Mitambo ya kuchakata zege pamoja na Mashine za kutengeneza tofali ambazo zitatumika kupunguza gharama za ujenzi katika miradi mbalimbali inayotekelezwa na TBA ukiwemo Mradi wa nyumba za makazi Magomeni Kota
Mji wa Serikali ambao ujenzi wake umesimamiwa na Wakala wa Majengo Tanzania (TBA), umezinduliwa rasmi Aprili 13, 2019 na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli ambaye amepongeza Taasisi zilizoshiriki kufanikisha ujenzi huo.
Watumishi wa Taasisi mbalimbali za Serikali mkoani Mbeya, wamevutiwa na Mradi wa nyumba za makazi – Bunju unaotekelezwa na Wakala wa Majengo Tanzania (TBA). Watumishi hao wameonyesha nia ya kuzinunua nyumba hizo baada ya uwasilishwaji uliofanywa na TBA katika Taasisi zao.