• Maswali
  • Wasiliana Nasi
  • English

Jamhuri ya Muungano wa TanzaniaWakala wa Majengo Tanzania

  • kuhusu Sisi
    • Ujumbe kutoka kwa Mtendaji Mkuu
    • Sisi ni Nani
    • Dira na Dhamira
    • Tunafanya Nini
    • Mikakati
    • Mkataba wa Huduma
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Bodi ya Ushauri
    • Muundo wa Taasisi
    • Senior Management
    • Kurugenzi wa Uwezeshaji wa Huduma
    • Kurugenzi ya Ushauri
    • Kurugenzi ya Ujenzi
    • Kurugenzi ya Miliki
    • Meneja wa Mikoa
  • Nyumba
    • Nyumba za Kuuza
    • Nyumba za Kupangisha
    • Fomu ya Ununuzi wa Nyumba
    • Fomu ya ununuzi wa Nyumba
  • Miradi
    • Miradi Tunayoishikilia
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Iliyo Katika usanifu
    • Miradi Tunayotegemea kufanya
  • Machapisho
    • Machapisho
  • Kituo Cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha
  • Ununuzi
    • Mpango wa Manunuzi wa Mwaka
    • Mialiko ya zabuni
    • Orodha ya Wazabuni Walioshinda

Habari Mpya

  • SERIKALI YAFUNGUA MILANGO YA UWEKEZAJI KWENYE UJENZI WA NYUMBA ZA MAKAZI

    tokea mwezi 1
  • MENEJIMENTI YA TBA YAHIMIZWA KUKUTANA MARA KWA MARA.

    tokea miezi 2
  • TBA YAKUTANA NA WAWEKEZAJI KUTOKA JAPAN.

    tokea miezi 2
  • TBA NA ZBA KUENDELEZA MASHIRIKIANO

    tokea miezi 2

Latest Press Release

ARCH. KONDORO AZINDUA MAFUNZO ELEKEZI YA BODI ZA ZABUNI

Imewekwa: Friday 02, December 2022

Desemba 1, 2022 Mtendaji Mkuu wa TBA Arch. Daud Kondoro amezindua Bodi ndogo za Zabuni za Kanda sita za TBA na alifungua mafunzo ya Bodi kuu, Bodi ndogo na Kitengo cha Manunuzi TBA, mafunzo hayo ambayo ni ya siku tatu yameanza tarehe 1 mpaka 3 Desemba mwaka huu katika ukumbu wa mikutano wa St. Gasper Jijini Dodoma.

Akizungumza wakati wa uzinduzi huo Arch. Kondoro amesisitiza wajumbe wa bodi hizo kutumia fursa ya mafunzo hayo kuongeza ufanisi na weledi.

"Kwa kushiriki mafunzo haya mtaweza kutekeleza kwa urahisi majukumu ya Wakala katika kusimamia Ununuzi wa Vifaa, Huduma na Kandarasi mbalimbali. Hivyo ni imani yetu kwamba kumalizika kwa mafunzo haya, kutakuwa si tu chachu ya utekelezaji wa majukumu ya Wakala bali tutaweka Dira na mwelekeo wa masuala ya msingi yenye matokeo makubwa yatakayotuongoza katika shughuli za Ununuzi na kuondoa mapungufu yote yaliyojitokeza huko nyuma ili tuweze kuendana na kasi ya mabadiliko ya Serikali ya Awamu ya Sita chini ya Uongozi shupavu wa Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania" amesema Arch.

Kondoro

Vile vile Arch. Kondoro amesema uwepo wa Bodi hizo ni kwa Muujibu wa Sheria za Manunuzi ya Umma.

" Bodi hizi zinaundwa kwa mujibu wa Kifungu cha 31 (1) cha Sheria ya ununuzi wa Umma ya mwaka 2011 na Kanuni zake za mwaka 2013 kinachoeleza kuwa kila Taasisi ya Serikali inapaswa kuwa na Bodi ya Zabuni itakayosimamia Ununuzi wa Bidhaa, Huduma, Kandarasi na Uondoaji wa vifaa. Kwa lugha rahisi, Bodi ya Zabuni ni chombo muhimu ambacho kinahakikisha kuwa utekelezaji wa Mpango wa Ununuzi na matumizi bora ya rasilimali fedha katika usimamizi makini wa Miradi mbalimbali inayotekelezwa na Wakala wa Majengo kwa kuzingatia maelekezo ya Serikali" amesema Arch. Kondoro.

Aidha, Arch. Kondoro amewataka wajumbe wa Bodi hiyo kuweka juhudi na maarifa yote mpaka hapo mafunzo hayo yatakapo malizika.

Mafunzo hayo yanatarajiwa kudumu kwa siku tatu ambapo yamehusisha wajumbe kutoka mikoa yote 26 Tanzania Bara ambayo TBA ina ofisi zake nchini.

Tanzania Census 2022

Mawasiliano yetu

TBA
THE CHIEF EXECUTIVE, TANZANIA BUILDINGS AGENCY (TBA), 13 MOROGORO ROAD, P.O BOX 94, 41102 VIWANDANI, DODOMA TANZANIA, EMAIL: ce@tba.go.tz Website: www.tba.go.tz
Nukushi :
Namba ya Simu : +255 733 483 437, +255 677 108 010
Barua Pepe : barua@tba.go.tz

Linki za Haraka

Linki Linganifu

  • WIZARA YA UJENZI NA UCHUKUZI
  • Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo
  • Utumishi
  • Tume ya Takwimu ya Taifa
  • Tume ya Ajira

©2025 wakala wa majengo tanzania . Haki zote zimehifadhiwa..

Imesanifiwa, Imetengenezwa na Mamlaka ya Serikali Mtandao.Inaendeshwa na Wakala ya Majengo Tanzania