• Maswali
  • Wasiliana Nasi
  • English

Jamhuri ya Muungano wa TanzaniaWakala ya Majengo Tanzania

  • kuhusu Sisi
    • Ujumbe kutoka kwa Mtendaji Mkuu
    • Sisi ni Nani
    • Dira na Dhamira
    • Tunafanya Nini
    • Mikakati
    • Mkataba wa Huduma
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Bodi ya Ushauri
    • Muundo wa Taasisi
    • Senior Management
    • Kurugenzi wa Uwezeshaji wa Huduma
    • Kurugenzi ya Ushauri
    • Kurugenzi ya Ujenzi
    • Kurugenzi ya Miliki
    • Meneja wa Mikoa
  • Nyumba
    • Nyumba za Kuuza
    • Nyumba za Kupangisha
    • Fomu ya Ununuzi wa Nyumba
    • Fomu ya ununuzi wa Nyumba
  • Miradi
    • Miradi Tunayoishikilia
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Iliyo Katika usanifu
    • Miradi Tunayotegemea kufanya
  • Machapisho
    • Machapisho
  • Kituo Cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Picha
    • Maktaba ya Video
  • Ununuzi
    • Mpango wa Manunuzi wa Mwaka
    • Mialiko ya zabuni
    • Orodha ya Wazabuni Walioshinda

Habari Mpya

  • KATIBU MKUU UJENZI AKAGUA UKARABATI NYUMBA ZA TBA DODOMA.

    tokea miezi 2
  • KATIBU MKUU WIZARA YA UJENZI ARCH. ELIUS MWAKALINGA ATEMBELEA NA KUKAGUA MAENDELEO YA MRADI WA MAGOMENI KOTA

    tokea miezi 4
  • RAIS MAGUFULI AMKABIDHI NYUMBA RAIS WA AWAMU YA PILI MHE. ALI HASSAN MWINYI

    tokea miezi 4
  • WAKUU WA WILAYA ZA NYANG’HWALE NA BIHARAMURO WATEMBELEA BANDA LA TBA

    tokea miezi 5

Latest Press Release

Ujumbe Kutoka kwa Mtendaji Mkuu

Wakala wa Majengo Tanzania (TBA), imejipambanua katika kutoa huduma bora na yenye kukidhi viwango vinavyostahili. Jukumu kuu la Wakala wa Majengo Tanzania ni Usimamizi na Uendeshaji wa Miliki yote ya Serikali nchini. Jukumu hili limegawanyika katika maeneo mawili makubwa. Huduma ya Ushauri, Huduma ya ushauri wa michoro na makabrasha yanayotumika pamoja na usimamizi ikiwemo ushauri wa Kisera/Miongozo ya majengo ya Serikali na Uendeshaji wa Miliki.

Kuhusu Usimamizi na Uendeshaji wa Miliki ya Serikali, TBA tumejikita katika kujenga na kuwauzia nyumba za Serikali Watumishi wa Umma, kujenga na kuwapangisha Watumishi wa Umma na wananchi wengine nyumba za Serikali, kutunza na kuweka kumbukumbu za takwimu za majengo yote ya Serikali, kuzifanyia matengenezo nyumba na majengo ya Serikali, kupata na kusimamia matumizi sahihi na endelevu ya viwanja vya Serikali pia Kununua na kuweka samani zenye ubora kwenye nyumba za Viongozi na majengo ya Serikali.

Hivyo kufuatia adhima hii, TBA tumejiwekea mikakati zaidi, kuhakikisha kuwa tunafanikisha miradi yote tunayotekeleza kwa kuzingatia ubora, gharama na muda wa kazi. Vyote hivi vinaendana na dhamani halisi ya pesa (Value for Money) tunayowekeza katika Miradi husika.

Kwa muktadha huo TBA, tumejitahidi kuhakikisha kuwa tunakuwa na Menejimenti nzuri ya Rasilimali watu ambayo imesheheni wataalamu wenye ujuzi na maarifa ya kutosha kulingana na sifa ya Taasisi yetu. Kama TBA tunahakikisha kuwa watumishi tulionao wanakuwa na maarifa na ujuzi sambamba na vitendea kazi vya kutosha, kwa hili TBA tumepiga hatua kwa kuweka mazingira mazuri ya utendaji kazi kwa watumishi wetu.

Pia TBA tumefanikiwa kununua vifaa vya kisasa vinavyosaidia kuleta ufanisi katika kazi. Vifaa hivi vinatuwezesha kujenga kwa haraka, ubora na uhakika na matokeo yake ni unafuu kwa umaliziaji, usimamizi na udhibiti wa ubora na gharama

Jambo lingine, ni suala la uwajibikaji yaani “Commitment”. Katika hili TBA tumejitahidi na bado tunaendelea kuhakikisha tunajenga moyo wa kujituma kwa wafanyakazi katika utendaji kazi. Hili ni suala ambalo TBA tumeliwekea mkazo mkubwa na kulipa kipau mbele. Tunaamini kuwa utaalamu na bidii ya kazi kwa kuzingatia maelekezo yanayotolewa, hivyo hali hii inachangia kujenga maadili na nidhamu nzuri ya kazi. Kazi bila nidhamu haiwezi kuwa bora na upungufu wa maadili unaharibu utendaji kazi.

Tukizungumzia zaidi kuhusu maadili, ni pamoja na kuwa na watumishi ambao wanafanya kazi kwa uaminifu. Kwa kutambua hilo, TBA tunajitahidi kutekeleza majukumu yetu kwa kuhakikisha kuwa tunazingatia mambo hayo makuu matatu ambayo ni utaalamu, bidii na maadili. Hii ndiyo nguzo yetu ya kufanikisha mikakati yetu.

Mawasiliano yetu

Wakala Ya Majengo Tanzania
Opposite karimjee Hall,P.O.Box 9542 Dar es Salaam Tanzania
Nukushi : +255 22 2114143
Namba ya Simu : +255 22 2122163/ 2117114
Barua Pepe : ce@tba.go.tz/ barua@tba.go.tz

Linki za Haraka

Linki Linganifu

  • Wizara ya Ujenzi,Uchukuzi na Mawasiliano
  • Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo
  • Utumishi
  • Tume ya Takwimu ya Taifa
  • Tume ya Ajira

©2021 wakala ya majengo tanzania . Haki zote zimehifadhiwa..

Imesanifiwa, Imetengenezwa na Mamlaka ya Serikali Mtandao.Inaendeshwa na Wakala ya Majengo Tanzania