• Maswali
  • Wasiliana Nasi
  • English

Jamhuri ya Muungano wa TanzaniaWakala wa Majengo Tanzania

  • kuhusu Sisi
    • Ujumbe kutoka kwa Mtendaji Mkuu
    • Sisi ni Nani
    • Dira na Dhamira
    • Tunafanya Nini
    • Mikakati
    • Mkataba wa Huduma
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Bodi ya Ushauri
    • Muundo wa Taasisi
    • Senior Management
    • Kurugenzi wa Uwezeshaji wa Huduma
    • Kurugenzi ya Ushauri
    • Kurugenzi ya Ujenzi
    • Kurugenzi ya Miliki
    • Meneja wa Mikoa
  • Nyumba
    • Nyumba za Kuuza
    • Nyumba za Kupangisha
    • Fomu ya Ununuzi wa Nyumba
    • Fomu ya ununuzi wa Nyumba
  • Miradi
    • Miradi Tunayoishikilia
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Iliyo Katika usanifu
    • Miradi Tunayotegemea kufanya
  • Machapisho
    • Machapisho
  • Kituo Cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha
  • Ununuzi
    • Mpango wa Manunuzi wa Mwaka
    • Mialiko ya zabuni
    • Orodha ya Wazabuni Walioshinda

Habari Mpya

  • SERIKALI YAFUNGUA MILANGO YA UWEKEZAJI KWENYE UJENZI WA NYUMBA ZA MAKAZI

    tokea mwezi 1
  • MENEJIMENTI YA TBA YAHIMIZWA KUKUTANA MARA KWA MARA.

    tokea mwezi 1
  • TBA YAKUTANA NA WAWEKEZAJI KUTOKA JAPAN.

    tokea mwezi 1
  • TBA NA ZBA KUENDELEZA MASHIRIKIANO

    tokea mwezi 1

Latest Press Release

NAIBU WAZIRI KASEKENYA ATEMBELEA MRADI WA UJENZI WA NYUMBA ZA MAKAZI - GHANA KOTA

Imewekwa: Thursday 24, August 2023

Naibu Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi Sekta ya Ujenzi Mhe. Mha. Godfrey Kasekenya ametembelea na kukagua maendeleo ya mradi wa ujenzi wa nyumba za makazi katika eneo la Ghana kota jijini Mwanza.

Kwa upande wa Naibu Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi Sekta ya Ujenzi Mha. Godfrey Kasekenya ameipongeza TBA kwa kazi nzuri na zenye ubora inazoendelea kuzifanya katika maeneo mbalimbali kama vile Dar es salaam (Temeke Kota, Magomeni Kota na Canadian), Arusha, na sasa mkoani Mwanza (Ghana Kota).

Pia Mhe. Kasekenya ameiagiza TBA kuhakikisha inamaliza mradi huo kwa wakati, kuzingatia ubora, viwango na gharama nafuu ili kujenga makazi yenye ubora wa hali ya juu kwa sababu jengo hilo linajengwa na kusimamiwa na TBA.

Aidha, Mhe. Kasekenya ameitaka TBA kushirikiana na Sekta binafsi pindi maboresho ya sheria ya kuanzisha TBA yatakapopitishwa ili kuhakikisha inajenga majengo mengi na yenye ubora kwa sababu TBA ina maeneo mengi yaliyo wazi hivyo itaweza kujenga majengo mengi zaidi ili kuendelea kukabiliana na uhaba wa nyumba nchini.

Awali akiwasilisha taarifa ya utekelezaji wa mradi huo, Kaimu Meneja wa TBA Mkoa wa Mwanza Mha. Moses Urio alisema utekelezaji wa mradi huo ni utekelezaji wa ilani ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) inayoitaka TBA kujenga nyumba za ghorofa ili kuchukua familia nyingi na kupunguza uhaba wa nyumba nchini.

Pia, Meneja Urio aliongeza kuwa mradi huo umeleta manufaa makubwa kwani umetoa ajira kwa mama lishe, mafundi na wanufaika takribani 70 kwa mwezi pamoja na kutoa mafunzo kwa vitendo kwa wanafunzi kutoka vyuo mbalimbali.

Ujenzi wa jengo hilo unatekelezwa na Wakala wa Majengo Tanzania (TBA) kwa kutumia fedha za ndani na pindi jengo hilo litakapokamilika litakuwa na uwezo wa kuchukua familia kumi na nne (14) pamoja na maduka 30 kwa ajili ya kutoa huduma za kijamii kwa wakazi watakaoishi kwenye nyumba hizo.

Tanzania Census 2022

Mawasiliano yetu

TBA
THE CHIEF EXECUTIVE, TANZANIA BUILDINGS AGENCY (TBA), 13 MOROGORO ROAD, P.O BOX 94, 41102 VIWANDANI, DODOMA TANZANIA, EMAIL: ce@tba.go.tz Website: www.tba.go.tz
Nukushi :
Namba ya Simu : +255 733 483 437, +255 677 108 010
Barua Pepe : barua@tba.go.tz

Linki za Haraka

Linki Linganifu

  • WIZARA YA UJENZI NA UCHUKUZI
  • Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo
  • Utumishi
  • Tume ya Takwimu ya Taifa
  • Tume ya Ajira

©2025 wakala wa majengo tanzania . Haki zote zimehifadhiwa..

Imesanifiwa, Imetengenezwa na Mamlaka ya Serikali Mtandao.Inaendeshwa na Wakala ya Majengo Tanzania