Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC) imetembelea na kukagua mradi wa ujenzi wa nyumba za Makazi ya Watumishi wa Umma wa Temeke Kota jijini Dar es Salaam.
Mara baada yakupokea taarifa ya utekelezaji wa mradi, Kamati hiyo ilitembelea eneo la mradi na kuona hatua iliyofikiwa katika utekelezaji wa mradi huo.
Akizungumza baada ya kutembelea mradi huo Makamu wa Mwenyekiti wa Kamati hiyo, Mhe. Isack Kamwelwe (Mb) amesema TBA inatekeleza mradi huo kwa fedha kutoka Serikalini.
"Ni muhumu jamaii ikaelewa kuwa kwa mwaka wa fedha 2022/23 TBA imepokea fedha kiasi cha shilingi bilioni 4.3 kwa ajili kuendelea na utekelezaji wa mradi huu. Aidha, fedha zilizotolewa na Serikali kwa wakati huu ni kwa ajili ya jengo moja la ghorofa tisa (9) lenye uwezo wa kuchukua familia 144”. amesema Kamwelwe.
Vile vile Mhe. Kamwelwe amesema Kamati imeridhishwa na hatua iliyofikia katika utekelezaji wa mradi huo na inatarajia kuwa Serikali itatoa fedha zitakazokamilisha mpango wa ujenzi kama ilivyokusudiwa pamoja na kuzingatia mahitaji msingi ya ujenzi wa mradi huo.
Kwa upande wake Mtendaji Mkuu wa TBA Arch. Daud Kondoro amesema TBA imewasilisha taarifa yake na kujadiliwa vyema na kamati hiyo ikiwa ni pamoja kupokea maelekezo kwa lengo la kufanikisha utekelezaji ambao umefikia 19%.
Mradi wa ujenzi wa nyumba za makazi kwa ajili ya Watumishi wa Umma katika eneo la Temeke Kota unatekelezwa na TBA kama Mkandarasi na Mshauri Elekezi.