• Maswali
  • Wasiliana Nasi
  • English

Jamhuri ya Muungano wa TanzaniaWakala wa Majengo Tanzania

  • kuhusu Sisi
    • Ujumbe kutoka kwa Mtendaji Mkuu
    • Sisi ni Nani
    • Dira na Dhamira
    • Tunafanya Nini
    • Mikakati
    • Mkataba wa Huduma
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Bodi ya Ushauri
    • Muundo wa Taasisi
    • Senior Management
    • Kurugenzi wa Uwezeshaji wa Huduma
    • Kurugenzi ya Ushauri
    • Kurugenzi ya Ujenzi
    • Kurugenzi ya Miliki
    • Meneja wa Mikoa
  • Nyumba
    • Nyumba za Kuuza
    • Nyumba za Kupangisha
    • Fomu ya Ununuzi wa Nyumba
    • Fomu ya ununuzi wa Nyumba
  • Miradi
    • Miradi Tunayoishikilia
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Iliyo Katika usanifu
    • Miradi Tunayotegemea kufanya
  • Machapisho
    • Machapisho
  • Kituo Cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha
  • Ununuzi
    • Mpango wa Manunuzi wa Mwaka
    • Mialiko ya zabuni
    • Orodha ya Wazabuni Walioshinda

Habari Mpya

  • SERIKALI YAFUNGUA MILANGO YA UWEKEZAJI KWENYE UJENZI WA NYUMBA ZA MAKAZI

    tokea mwezi 1
  • MENEJIMENTI YA TBA YAHIMIZWA KUKUTANA MARA KWA MARA.

    tokea miezi 2
  • TBA YAKUTANA NA WAWEKEZAJI KUTOKA JAPAN.

    tokea miezi 2
  • TBA NA ZBA KUENDELEZA MASHIRIKIANO

    tokea miezi 2

Latest Press Release

PROF. MBARAWA AZINDUA RASMI BODI YA USHAURI YA TBA

Imewekwa: Friday 22, July 2022

Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, Prof. Makame Mbarawa (Mb) ameitaka Bodi Mpya ya Ushauri ya Wakala wa Majengo Tanzania (TBA), kuuwezesha Wakala huo kuwekeza kikamilifu katika viwanja vyake vilivyopo katika maeneo ya kimkakati ili kumaliza tatizo la upungufu wa nyumba za viongozi na watumishi wa umma lililopo nchini.

Akizungumza mara baada ya kuzindua Bodi hiyo jijini Dar es Salaam, Prof. Mbarawa amesema huu ndio wakati wa TBA kujiimarisha kimiundombinu na kiuchumi kwa kutumia fursa ya mahitaji ya nyumba kwa ajili ya watumishi wa umma na majengo ya kibiashara katika miji mikuu.

"..Hakikisheni mnakuja na mipango ya kutumia rasilimali ya viwanja na majengo mlio nayo kupata faida kwa kujenga majengo mazuri katika maeneo ya miji na kuhakikisha nyumba zenu zaidi ya elfu sita zilizopo zinakuwa katika viwango bora wakati wote na kuvutia wapangaji," amesema Prof. Mbarawa.

Prof. Mbarawa ameipongeza TBA, kwa mradi wa ujenzi wa nyumba za watumishi 3,500 Nzuguni Jijini Dodoma na kuongeza kuwa mradi huo ukikamilika kwa wakati utawaongezea mapato kwa kuwa bado mahitaji ya nyumba za viongozi na watumishi wa umma katika maeneo ya mijini ni makubwa.

"...Tengenezeni mikakati ya ubunifu itakayo wawezesha kushirikiana na sekta binafsi ili kuhakikisha sekta ya majenzi na makazi ya viongozi na watumishi wa umma inaimarika," amesisitiza Prof. Mbarawa.

Kwa upande wake, Mwenyekiti wa Bodi ya Ushauri ya TBA, Arch. Dk. Ombeni Swai amesema Bodi yake itafanya kazi kwa uadilifu na ubunifu ili kuiwezesha TBA kupata faida na kutoa huduma ya kuaminika kwa Watanzania.

Naye Mtendaji Mkuu wa TBA, Arch. Daud Kondoro amemshukuru Waziri Prof. Mbarawa kwa miongozo anayoitoa na kusisitiza kuwa TBA itaendelea kusimamia mifumo, nidhamu, udhibiti na uendelezaji wa miradi mbalimbali ya nyumba na majengo ya Serikali nchini kote kwa kuzingatia mahitaji na faida ili kukuza mtaji ikiwemo ujenzi wa nyumba 3,500 jijini Dodoma.

Wajumbe wapya wa Bodi ya Ushauri ya TBA itakayohudumu kwa miaka mitatu ni pamoja na Arch. Dk. Ombeni Swai (Mwenyekiti), Qs. Optatus Kanyesi (Mjumbe), Bw. Shaban Kabunga (Mjumbe), Qs. Joseph Mkali (Mjumbe), na Bi. Vicky Jengo (Mjumbe).


Tanzania Census 2022

Mawasiliano yetu

TBA
THE CHIEF EXECUTIVE, TANZANIA BUILDINGS AGENCY (TBA), 13 MOROGORO ROAD, P.O BOX 94, 41102 VIWANDANI, DODOMA TANZANIA, EMAIL: ce@tba.go.tz Website: www.tba.go.tz
Nukushi :
Namba ya Simu : +255 733 483 437, +255 677 108 010
Barua Pepe : barua@tba.go.tz

Linki za Haraka

Linki Linganifu

  • WIZARA YA UJENZI NA UCHUKUZI
  • Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo
  • Utumishi
  • Tume ya Takwimu ya Taifa
  • Tume ya Ajira

©2025 wakala wa majengo tanzania . Haki zote zimehifadhiwa..

Imesanifiwa, Imetengenezwa na Mamlaka ya Serikali Mtandao.Inaendeshwa na Wakala ya Majengo Tanzania