• Maswali
  • Wasiliana Nasi
  • English

Jamhuri ya Muungano wa TanzaniaWakala wa Majengo Tanzania

  • kuhusu Sisi
    • Ujumbe kutoka kwa Mtendaji Mkuu
    • Sisi ni Nani
    • Dira na Dhamira
    • Tunafanya Nini
    • Mikakati
    • Mkataba wa Huduma
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Bodi ya Ushauri
    • Muundo wa Taasisi
    • Senior Management
    • Kurugenzi wa Uwezeshaji wa Huduma
    • Kurugenzi ya Ushauri
    • Kurugenzi ya Ujenzi
    • Kurugenzi ya Miliki
    • Meneja wa Mikoa
  • Nyumba
    • Nyumba za Kuuza
    • Nyumba za Kupangisha
    • Fomu ya Ununuzi wa Nyumba
    • Fomu ya ununuzi wa Nyumba
  • Miradi
    • Miradi Tunayoishikilia
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Iliyo Katika usanifu
    • Miradi Tunayotegemea kufanya
  • Machapisho
    • Machapisho
  • Kituo Cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha
  • Ununuzi
    • Mpango wa Manunuzi wa Mwaka
    • Mialiko ya zabuni
    • Orodha ya Wazabuni Walioshinda

Habari Mpya

  • SERIKALI YAFUNGUA MILANGO YA UWEKEZAJI KWENYE UJENZI WA NYUMBA ZA MAKAZI

    tokea mwezi 1
  • MENEJIMENTI YA TBA YAHIMIZWA KUKUTANA MARA KWA MARA.

    tokea miezi 2
  • TBA YAKUTANA NA WAWEKEZAJI KUTOKA JAPAN.

    tokea miezi 2
  • TBA NA ZBA KUENDELEZA MASHIRIKIANO

    tokea miezi 2

Latest Press Release

RAIS SAMIA AWEKA JIWE LA MSINGI MRADI WA UJENZI WA OFISI YA MKUU WA MKOA WA MBEYA

Imewekwa: Tuesday 09, August 2022

Agosti 05, 2022 Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan ametembelea na kuweka jiwe la Msingi kwenye Mradi wa Ujenzi wa Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mbeya iliyobuniwa na kujengwa na Wakala wa Majengo Tanzania (TBA).

Baada ya kuweka jiwe la msingi Mhe. Rais Samia amepongeza jitihada zilizochukuliwa katika utekelezaji wa mradi huo kwa kuwa utakwenda kusaidia wakazi wa Mbeya kupata huduma bora za kiutawala.

Aidha Mhe. Rais Samia amesema amezunguka Mikoa mingi na kuona majengo ya Wakuu wa Mikoa mbalimbali lakini jengo la Mkuu wa Mkoa wa Mbeya lililobuniwa na kujengwa na TBA ni la aina yake kutokana na ubora na uzuri wa jengo hilo.

Hata hivyo, Mhe Rais Samia amesifia kazi nzuri ambayo imefanywa na Wakala wa Majengo Tanzania (TBA) katika kuhakikisha shughuli ya Serikali ya Utawala Bora inatekelezwa vyema katika kuboresha maeneo ambayo wananchi wataweza kuhudumiwa.

Mhe. Rais pia amesisitiza kuwa Serikali itaendelea kujenga Majengo makubwa ya aina hiyo katika mikoa mbalimbali hasa maeneo ya Makao Makuu ya Kanda.

Akizungumza na TBC1 baada ya kuweka jiwe la msingi, Mtendaji Mkuu wa TBA Arch. Daud Kondoro amemshukuru Mhe. Rais Samia kwa kuweka jiwe la msingi.

"Kwanza namshukuru Mheshimiwa Rais Samia kuweka jiwe la msingi, hii inaashiria jengo limekidhi viwango vya ubora na utekelezaji wa Mradi huu kwa TBA ni wajibu kwa sababu Wakala una jukumu la kusimamia Miliki za Serikali ikiwemo Ofisi na nyumba za Serikali na kuhakikisha Watumishi wanakaa katika makazi ambayo ni salama ambayo yanaweza kuleta tija katika kutoa huduma" alisema Arch. Kondoro.

Akizungumza juu ya ubora wa jengo la ofisi ya Mkuu wa Mkoa ya Mbeya Arch. Kondoro amesema kuwa TBA imefuata taratibu zote ikiwa ni pamoja na kupima malighafi zote za ujenzi ili kujiridhisha na viwango vya ubora.

Aidha, Arch. Kondoro amezungumzia ushiriki wa TBA katika mradi wa ujenzi wa Mji wa Serikali katika eneo la Mtumba Jijini Dodoma."Unafahamu kuwa kuna ujenzi unaendelea sasa wa Mji wa Serikali awamu ya pili ambapo ubunifu wa mji ule umefanywa na TBA lakini pia tunajenga baadhi ya Majengo" alisema Arch. Kondoro.

Mradi wa ujenzi wa jengo la Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mbeya unatekelezwa na TBA kama Mkandarasi na kusimamiwa na MUST kama Mshauri Elekezi ambapo uwekaji wa Jiwe la Msingi la ujenzi wa mradi huo umefanywa na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Samia Suluhu Hassan Agosti 5, 2022.

Tanzania Census 2022

Mawasiliano yetu

TBA
THE CHIEF EXECUTIVE, TANZANIA BUILDINGS AGENCY (TBA), 13 MOROGORO ROAD, P.O BOX 94, 41102 VIWANDANI, DODOMA TANZANIA, EMAIL: ce@tba.go.tz Website: www.tba.go.tz
Nukushi :
Namba ya Simu : +255 733 483 437, +255 677 108 010
Barua Pepe : barua@tba.go.tz

Linki za Haraka

Linki Linganifu

  • WIZARA YA UJENZI NA UCHUKUZI
  • Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo
  • Utumishi
  • Tume ya Takwimu ya Taifa
  • Tume ya Ajira

©2025 wakala wa majengo tanzania . Haki zote zimehifadhiwa..

Imesanifiwa, Imetengenezwa na Mamlaka ya Serikali Mtandao.Inaendeshwa na Wakala ya Majengo Tanzania