• Maswali
  • Wasiliana Nasi
  • English

Jamhuri ya Muungano wa TanzaniaWakala wa Majengo Tanzania

  • kuhusu Sisi
    • Ujumbe kutoka kwa Mtendaji Mkuu
    • Sisi ni Nani
    • Dira na Dhamira
    • Tunafanya Nini
    • Mikakati
    • Mkataba wa Huduma
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Bodi ya Ushauri
    • Muundo wa Taasisi
    • Senior Management
    • Kurugenzi wa Uwezeshaji wa Huduma
    • Kurugenzi ya Ushauri
    • Kurugenzi ya Ujenzi
    • Kurugenzi ya Miliki
    • Meneja wa Mikoa
  • Nyumba
    • Nyumba za Kuuza
    • Nyumba za Kupangisha
    • Fomu ya Ununuzi wa Nyumba
    • Fomu ya ununuzi wa Nyumba
  • Miradi
    • Miradi Tunayoishikilia
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Iliyo Katika usanifu
    • Miradi Tunayotegemea kufanya
  • Machapisho
    • Machapisho
  • Kituo Cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha
  • Ununuzi
    • Mpango wa Manunuzi wa Mwaka
    • Mialiko ya zabuni
    • Orodha ya Wazabuni Walioshinda

Habari Mpya

  • SERIKALI YAFUNGUA MILANGO YA UWEKEZAJI KWENYE UJENZI WA NYUMBA ZA MAKAZI

    tokea mwezi 1
  • MENEJIMENTI YA TBA YAHIMIZWA KUKUTANA MARA KWA MARA.

    tokea mwezi 1
  • TBA YAKUTANA NA WAWEKEZAJI KUTOKA JAPAN.

    tokea mwezi 1
  • TBA NA ZBA KUENDELEZA MASHIRIKIANO

    tokea mwezi 1

Latest Press Release

WADAIWA SUGU NYUMBA ZA TBA DODOMA WAANZA KUONDOLEWA.

Imewekwa: Monday 11, December 2023

Operesheni ya kuwaondoa wadaiwa sugu katika nyumba za Wakala wa Majengo Tanzania (TBA), imeendelea kutekelezwa katika mkoa wa Dodoma. Utekelezwaji wake unahusisha kuwaondoa wadaiwa sugu, watu wanaoishi katika nyumba za TBA kinyume na utaratibu ambao si wapangaji halali pamoja na watu wengine waliojimilikisha mali za TBA zikiwemo nyumba na viwanja pasipo halali.

Akizungumzia zoezi hili, Kaimu Meneja wa TBA mkoa wa Dodoma Arch. Vilumba Sanga amesema, zoezi litakuwa endelevu hadi pale wadaiwa wote watakapokuwa wamelipa madeni yao.

"Pamoja na wadaiwa sugu lakini pia kuna baadhi ya wapangaji hawaishi kwenye nyumba hizo badala yake wameweka watu wengine wanaishi pasipo halali, kinyume na utaratibu unaotakiwa, tutawaondoa wote na madeni wanayodaiwa lazima wayalipe kwa mujibu wa mkataba" Amesisitiza Arch. Sanga

Aidha, Arch. Sanga, ametoa wito kwa wapangaji wote kuzingatia utaratibu wa kimkataba, kulipa kodi kwa wakati, kutolimbikiza kodi na kuachiana nyumba kiholela pasipo kufuata utaratibu.

Naye, Mkurugenzi wa Kampuni ya Twins Auction Mart, ambao ndiyo walioshinda zabuni ya kuwaondoa wapangaji hao kwa taratibu za Mahakama, Bw. Zuberi Hassan, amebainisha kuwa zoezi linakwenda vizuri na watahakikisha kuwa wadaiwa wote wanaondolewa kwenye nyumba hizo na kulipa madeni yao.

Tanzania Census 2022

Mawasiliano yetu

TBA
THE CHIEF EXECUTIVE, TANZANIA BUILDINGS AGENCY (TBA), 13 MOROGORO ROAD, P.O BOX 94, 41102 VIWANDANI, DODOMA TANZANIA, EMAIL: ce@tba.go.tz Website: www.tba.go.tz
Nukushi :
Namba ya Simu : +255 733 483 437, +255 677 108 010
Barua Pepe : barua@tba.go.tz

Linki za Haraka

Linki Linganifu

  • WIZARA YA UJENZI NA UCHUKUZI
  • Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo
  • Utumishi
  • Tume ya Takwimu ya Taifa
  • Tume ya Ajira

©2025 wakala wa majengo tanzania . Haki zote zimehifadhiwa..

Imesanifiwa, Imetengenezwa na Mamlaka ya Serikali Mtandao.Inaendeshwa na Wakala ya Majengo Tanzania