• Maswali
  • Wasiliana Nasi
  • English

Jamhuri ya Muungano wa TanzaniaWakala wa Majengo Tanzania

  • kuhusu Sisi
    • Ujumbe kutoka kwa Mtendaji Mkuu
    • Sisi ni Nani
    • Dira na Dhamira
    • Tunafanya Nini
    • Mikakati
    • Mkataba wa Huduma
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Bodi ya Ushauri
    • Muundo wa Taasisi
    • Senior Management
    • Kurugenzi wa Uwezeshaji wa Huduma
    • Kurugenzi ya Ushauri
    • Kurugenzi ya Ujenzi
    • Kurugenzi ya Miliki
    • Meneja wa Mikoa
  • Nyumba
    • Nyumba za Kuuza
    • Nyumba za Kupangisha
    • Fomu ya Ununuzi wa Nyumba
    • Fomu ya ununuzi wa Nyumba
  • Miradi
    • Miradi Tunayoishikilia
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Iliyo Katika usanifu
    • Miradi Tunayotegemea kufanya
  • Machapisho
    • Machapisho
  • Kituo Cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha
  • Ununuzi
    • Mpango wa Manunuzi wa Mwaka
    • Mialiko ya zabuni
    • Orodha ya Wazabuni Walioshinda

Habari Mpya

  • SERIKALI YAFUNGUA MILANGO YA UWEKEZAJI KWENYE UJENZI WA NYUMBA ZA MAKAZI

    tokea mwezi 1
  • MENEJIMENTI YA TBA YAHIMIZWA KUKUTANA MARA KWA MARA.

    tokea miezi 2
  • TBA YAKUTANA NA WAWEKEZAJI KUTOKA JAPAN.

    tokea miezi 2
  • TBA NA ZBA KUENDELEZA MASHIRIKIANO

    tokea miezi 2

Latest Press Release

TBA IMEENDELEA NA UKARABATI WA NYUMBA WILAYANI MBOZI.

Imewekwa: Monday 15, August 2022

Wakala wa Majengo Tanzania (TBA) umeendelea na mpango maalumu wa ukaratabati wa nyumba na majengo katika maeneo mbalimbali nchini lengo likiwa ni kuboresha makazi na kuongeza ufanisi kwa Watumishi wa Umma ambao ndiyo wapangaji wa nyumba hizo. TBA imeendelea na jitihada hizo za ukarabati ambao unahusisha ukarabati wa paa, kupaka rangi, mifumo ya maji safi na taka Pamoja na ukarabati wa miundombinu ya umeme.

Mkoa wa Songwe ni miongoni mwa mikoa ambayo imenufaika na ukarabati huo ambapo ukaratabati unafanyika katika Wilaya ya Mbozi, kata ya Ichenjezya. Akizungumza juu ya ukarabati huo Afisa Miliki wa TBA Mkoani Songwe Bw. Thomas Mwasalyanda amesema katika eneo hilo kuna jumla ya nyumba kumi na mbili (12) ambazo zinabeba familia ishirini (20). “Ukarabati huu ulianza Februari, 2022 ambapo tulianza kufanya marekebisho ya paa, ikumbukwe pia hakukua na marumaru (tiles) katika maeneo ya jikoni, bafuni na chooni lakini kupitia ukarabati huu tumefanikisha kuweka marumaru. Vile vile tumefanikisha kuboresha miundombinu ya umeme ambapo kwa sasa kila nyumba imekuwa na mita ya luku pamoja na kuboresha upatikanaji wa maji ya uhakika kwa kuchimba kisima katika eneo hilo” amesema Mwasalyanda.

Vile vile Bw. Mwasalyanda amezungumzia juu ya ubora wa ukarabati huo ambapo amesema umezingatia taratibu zote katika maeneo yaliyofanyiwa ukarabati kwa kuondoa vifaa vyote vilivyokuwa vimechakaa na kuweka vifaa vinavyokidhi viwango vya ubora na ambavyo vitadumu kwa muda mrefu zaidi.

Bibi Mariam Shaban ni miongoni wa wakaazi wa eneo wa hilo ambaye amezungumzia ukarabati huo "kwa kweli tumefurahi kwa kufanyiwa ukarabati huu kwa sababu nyumba zinavyoonekana sasa ni tofauti na zilivyokuwa awali. Lakini jambo kubwa tunaloweza kuishukuru TBA ni kutuwekea maji ya uhakika kwa kuchimba kisima ambacho kinasambaza maji katika nyumba zote hizi na maji hayo yanapatikana wakati wote” amesema bibi Mariam.

Utekelezaji wa mpango wa ukarabati katika Wilaya Mbozi, kata ya Ichenjezya kwa sasa umefikia asilimia 80 za utekelezaji ambapo kazi mbalimbali zimekamilika. Vile vile ukarabati huo unatarajia kuendelea kufanyika katika wilaya ya Ileje katika Mkoa huo wa Songwe kwa lengo la kuboresha makazi ya watumishi wa umma.

Tanzania Census 2022

Mawasiliano yetu

TBA
THE CHIEF EXECUTIVE, TANZANIA BUILDINGS AGENCY (TBA), 13 MOROGORO ROAD, P.O BOX 94, 41102 VIWANDANI, DODOMA TANZANIA, EMAIL: ce@tba.go.tz Website: www.tba.go.tz
Nukushi :
Namba ya Simu : +255 733 483 437, +255 677 108 010
Barua Pepe : barua@tba.go.tz

Linki za Haraka

Linki Linganifu

  • WIZARA YA UJENZI NA UCHUKUZI
  • Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo
  • Utumishi
  • Tume ya Takwimu ya Taifa
  • Tume ya Ajira

©2025 wakala wa majengo tanzania . Haki zote zimehifadhiwa..

Imesanifiwa, Imetengenezwa na Mamlaka ya Serikali Mtandao.Inaendeshwa na Wakala ya Majengo Tanzania