• Maswali
  • Wasiliana Nasi
  • English

Jamhuri ya Muungano wa TanzaniaWakala wa Majengo Tanzania

  • kuhusu Sisi
    • Ujumbe kutoka kwa Mtendaji Mkuu
    • Sisi ni Nani
    • Dira na Dhamira
    • Tunafanya Nini
    • Mikakati
    • Mkataba wa Huduma
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Bodi ya Ushauri
    • Muundo wa Taasisi
    • Senior Management
    • Kurugenzi wa Uwezeshaji wa Huduma
    • Kurugenzi ya Ushauri
    • Kurugenzi ya Ujenzi
    • Kurugenzi ya Miliki
    • Meneja wa Mikoa
  • Nyumba
    • Nyumba za Kuuza
    • Nyumba za Kupangisha
    • Fomu ya Ununuzi wa Nyumba
    • Fomu ya ununuzi wa Nyumba
  • Miradi
    • Miradi Tunayoishikilia
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Iliyo Katika usanifu
    • Miradi Tunayotegemea kufanya
  • Machapisho
    • Machapisho
  • Kituo Cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha
  • Ununuzi
    • Mpango wa Manunuzi wa Mwaka
    • Mialiko ya zabuni
    • Orodha ya Wazabuni Walioshinda

Habari Mpya

  • SERIKALI YAFUNGUA MILANGO YA UWEKEZAJI KWENYE UJENZI WA NYUMBA ZA MAKAZI

    tokea mwezi 1
  • MENEJIMENTI YA TBA YAHIMIZWA KUKUTANA MARA KWA MARA.

    tokea miezi 2
  • TBA YAKUTANA NA WAWEKEZAJI KUTOKA JAPAN.

    tokea miezi 2
  • TBA NA ZBA KUENDELEZA MASHIRIKIANO

    tokea miezi 2

Latest Press Release

TBA KUSAIDIA UJENZI NA UKARABATI WA OFISI NA MADARASA SHULE YA SEKONDARI JUHUDI.

Imewekwa: Friday 28, February 2020

Wakala wa Majengo Tanzania (TBA), umeahidi kusaidia Ujenzi na Ukarabati wa Majengo katika Shule ya Sekondari Juhudi iliyopo eneo la Gongo la Mboto, Ilala Jijini Dar es Salaam. Shule hiyo iliyoanzishwa na kuendelezwa na wananchi wa eneo hilo, inakabiliwa na uchakavu wa miundo mbinu ya majengo kama ofisi na madarasa, hivyo kuwafanya wanafunzi na walimu kusoma na kufanya kazi katika mazingira magumu.

Akizungumza katika Mahafali ya Tatu ya Kidato cha Sita baada ya kusikiliza Risala iliyosomwa na Mkuu wa Shule pamoja na Risala iliyosomwa na viongozi wa Serikali ya Wanafunzi, Kaimu Mtendaji Mkuu wa TBA Bw. Said Mndeme aliyekuwa Mgeni Rasmi katika Mahafali hayo alisema, “TBA kama mdau wa sekta ya elimu upande wa miundo mbinu ya majengo na majenzi tutakarabati majengo ya Utawala na Ofisi za walimu pamoja na Madarasa 10 ya wanafunzi”. Pia aliahidi kujenga Ofisi kwa ajili ya serikali ya wanafunzi ambao wanafanya kazi bila kuwa na ofisi kwa sasa.

Shughuli ya Ukarabati imeshaanza kwa hatua za awali kwani mgeni rasmi aliambatana na jopo la wataalamu kutoka TBA ambao kabla ya kuanza kwa mahafali walitembelea na kuanza kufanya tathmini ya majengo yanayohitaji ukarabati.

Shule ya Sekondari Juhudi inaibua na kuendeleza vipaji vya wanafunzi katika Sekta ya Michezo lakini inakabiliwa na changamoto ya kukosa viwanja na miundo mbinu mingine ya michezo. Katika sherehe hizo za mahafali Mgeni Rasmi aliahidi kulifikisha suala hilo kwa wadau mbalimbali wa michezo ili walishughulikie.

Tanzania Census 2022

Mawasiliano yetu

TBA
THE CHIEF EXECUTIVE, TANZANIA BUILDINGS AGENCY (TBA), 13 MOROGORO ROAD, P.O BOX 94, 41102 VIWANDANI, DODOMA TANZANIA, EMAIL: ce@tba.go.tz Website: www.tba.go.tz
Nukushi :
Namba ya Simu : +255 733 483 437, +255 677 108 010
Barua Pepe : barua@tba.go.tz

Linki za Haraka

Linki Linganifu

  • WIZARA YA UJENZI NA UCHUKUZI
  • Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo
  • Utumishi
  • Tume ya Takwimu ya Taifa
  • Tume ya Ajira

©2025 wakala wa majengo tanzania . Haki zote zimehifadhiwa..

Imesanifiwa, Imetengenezwa na Mamlaka ya Serikali Mtandao.Inaendeshwa na Wakala ya Majengo Tanzania