• Maswali
  • Wasiliana Nasi
  • English

Jamhuri ya Muungano wa TanzaniaWakala wa Majengo Tanzania

  • kuhusu Sisi
    • Ujumbe kutoka kwa Mtendaji Mkuu
    • Sisi ni Nani
    • Dira na Dhamira
    • Tunafanya Nini
    • Mikakati
    • Mkataba wa Huduma
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Bodi ya Ushauri
    • Muundo wa Taasisi
    • Senior Management
    • Kurugenzi wa Uwezeshaji wa Huduma
    • Kurugenzi ya Ushauri
    • Kurugenzi ya Ujenzi
    • Kurugenzi ya Miliki
    • Meneja wa Mikoa
  • Nyumba
    • Nyumba za Kuuza
    • Nyumba za Kupangisha
    • Fomu ya Ununuzi wa Nyumba
    • Fomu ya ununuzi wa Nyumba
  • Miradi
    • Miradi Tunayoishikilia
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Iliyo Katika usanifu
    • Miradi Tunayotegemea kufanya
  • Machapisho
    • Machapisho
  • Kituo Cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha
  • Ununuzi
    • Mpango wa Manunuzi wa Mwaka
    • Mialiko ya zabuni
    • Orodha ya Wazabuni Walioshinda

Habari Mpya

  • SERIKALI YAFUNGUA MILANGO YA UWEKEZAJI KWENYE UJENZI WA NYUMBA ZA MAKAZI

    tokea mwezi 1
  • MENEJIMENTI YA TBA YAHIMIZWA KUKUTANA MARA KWA MARA.

    tokea miezi 2
  • TBA YAKUTANA NA WAWEKEZAJI KUTOKA JAPAN.

    tokea miezi 2
  • TBA NA ZBA KUENDELEZA MASHIRIKIANO

    tokea miezi 2

Latest Press Release

TBA YAINGIA SIKU YA NNE YA KUKABIDHI NYUMBA KWA WAKAZI 644 WA MAGOMENI KOTA.

Imewekwa: Friday 01, April 2022

Ikiwa imetimia siku ya nne tangu kuanza kwa zoezi la kukabidhi nyumba kwa wakazi 644 wa Magomeni Kota linaloratibiwa na Wakala wa Majengo Tanzania (TBA), idadi kubwa ya wakaazi wameendelea kujitokeza kwa ajili ya kukamilisha taratibu mbalimbali ili kukabidhiwa nyumba hizo, jambo linatoa taswira nzuri kuwa zoezi

linakwenda vizuri.

Akizungumza kwa niaba ya Wakala wa Majengo Tanzania TBA, Kaimu Meneja Mawasiliano kwa Umma na Masoko Bw. Fredrick Kalinga ameendelea kutoa taarifa juu ya zoezi hilo kuwa linakwenda vizuri na mpaka kufikia Machi 31, 2022 jumla ya kaya 306 kati ya kaya 644 zilikuwa zimeshapangiwa nyumba zao. "Leo Aprili 1 zoezi linaendelea na wakaazi wanaendelea kuonesha mwitikio mzuri hivyo tunategemea zoezi litakamilika ndani ya muda uliopangwa" aliongeza Bw. Kalinga

Wakiongea kwa nyakati tofauti wakaazi hawa wameonesha imani kubwa juu ya zoezi zima la ugawaji wa nyumba hizo kama asemavyo Bw. Majid Salum Mteleke “Hakuna matatizo yoyote, hitilafu ndogo ndogo ni vitu vya kawaida ukweli unabaki palepale kwamba kazi iliyofanyika ni nzuri sana”.

Aidha Bibi Sinahila Ramadhani hakuweza kuficha furaha yake baada ya kuiona nyumba yake na kusema “Nyumba ni ya kisasa sana,vitu vyote humu ndani ni vya kisasa yaani ujenzi huu umezingatia usasa wa ujenzi wa kipindi hiki tunashukuru sana sana Serikali ya Mama Samia Suluhu Hassan pamoja na Wakala wa Majengo (TBA) kwa nyumba hizi nzuri”. Wakiendelea kuonesha nia ya dhati ya kutunza makazi hayo, Bw. Majid Salum Mtekele aliongeza kwa kusema “hivyo walivyotutengenezea basi na sisi tuishi kwa hali tunayoiona tusiende tofauti.”

Zoezi la kuwapangia nyumba Wakaazi 644 wa Magomeni Kota linatarajia kuchukua takribani siku kumi tangu kuanza kwake 29 Machi, 2022.

Tanzania Census 2022

Mawasiliano yetu

TBA
THE CHIEF EXECUTIVE, TANZANIA BUILDINGS AGENCY (TBA), 13 MOROGORO ROAD, P.O BOX 94, 41102 VIWANDANI, DODOMA TANZANIA, EMAIL: ce@tba.go.tz Website: www.tba.go.tz
Nukushi :
Namba ya Simu : +255 733 483 437, +255 677 108 010
Barua Pepe : barua@tba.go.tz

Linki za Haraka

Linki Linganifu

  • WIZARA YA UJENZI NA UCHUKUZI
  • Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo
  • Utumishi
  • Tume ya Takwimu ya Taifa
  • Tume ya Ajira

©2025 wakala wa majengo tanzania . Haki zote zimehifadhiwa..

Imesanifiwa, Imetengenezwa na Mamlaka ya Serikali Mtandao.Inaendeshwa na Wakala ya Majengo Tanzania