• Maswali
  • Wasiliana Nasi
  • English

Jamhuri ya Muungano wa TanzaniaWakala wa Majengo Tanzania

  • kuhusu Sisi
    • Ujumbe kutoka kwa Mtendaji Mkuu
    • Sisi ni Nani
    • Dira na Dhamira
    • Tunafanya Nini
    • Mikakati
    • Mkataba wa Huduma
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Bodi ya Ushauri
    • Muundo wa Taasisi
    • Senior Management
    • Kurugenzi wa Uwezeshaji wa Huduma
    • Kurugenzi ya Ushauri
    • Kurugenzi ya Ujenzi
    • Kurugenzi ya Miliki
    • Meneja wa Mikoa
  • Nyumba
    • Nyumba za Kuuza
    • Nyumba za Kupangisha
    • Fomu ya Ununuzi wa Nyumba
    • Fomu ya ununuzi wa Nyumba
  • Miradi
    • Miradi Tunayoishikilia
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Iliyo Katika usanifu
    • Miradi Tunayotegemea kufanya
  • Machapisho
    • Machapisho
  • Kituo Cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha
  • Ununuzi
    • Mpango wa Manunuzi wa Mwaka
    • Mialiko ya zabuni
    • Orodha ya Wazabuni Walioshinda

Habari Mpya

  • SERIKALI YAFUNGUA MILANGO YA UWEKEZAJI KWENYE UJENZI WA NYUMBA ZA MAKAZI

    tokea mwezi 1
  • MENEJIMENTI YA TBA YAHIMIZWA KUKUTANA MARA KWA MARA.

    tokea miezi 2
  • TBA YAKUTANA NA WAWEKEZAJI KUTOKA JAPAN.

    tokea miezi 2
  • TBA NA ZBA KUENDELEZA MASHIRIKIANO

    tokea miezi 2

Latest Press Release

TBA YAJIVUNIA KUWEZESHA WANAFUNZI KUFANYA MAZOEZI KWA VITENDO

Imewekwa: Tuesday 06, September 2022

WAKALA wa Majengo Tanzania (TBA) unajivunia kuwapa nafasi wanafunzi kutoka vyuo mbalimbali nchini kufanya mazoezi kwa Vitendo (Field attachment) katika miradi yake inayotekeleza mkoani Dodoma. Baadhi ya miradi mikubwa ya kimkakati ambayo TBA inatekeleza mkoani humo, ni ujenzi wa Mji wa Serikali, ujenzi wa nyumba 3500 za watumishi wa umma katika eneo la Nzuguni B, ujenzi wa nyuma za viongozi sambamba na ujenzi wa ofisi zingine za Serikali katika maeneo mbalimbali Dodoma.

Afisa Rasilimali watu ofisi ya TBA mkoa wa Dodoma, Bi Nashira Iddi anasema, tokea mwezi Januari hadi Septemba 2022, jumla ya wanafunzi 50 wamepokelewa na kufanya mafunzo kwa vitendo katika miradi hiyo.

“TBA tumeendelea kupokea wanafunzi kutoka vyuo mbalimbali kuja kujifunza kwa vitendo kwenye miradi yetu hapa Dodoma, tunaamini kuwa mafunzo hayo yatawasaidia katika taaluma zao.” Anabainisha Nashira

Patricia Olomi, ambaye ni mwanafunzi wa chuo kikuu cha Dar es Salaam (UDSM), anayesomea Uhandisi ujenzi anasema, mafunzo hayo kwa vitendo yanawasaidia yanawaongezea maarifa na ujuzi katika fani zao.

Naye Brian Mushi, mwanafunzi wa chuo kikuu cha Ardhi, ambaye anasomea upimaji ardhi, amebainisha kuwa tangu wahudhurie mafunzo hayo, TBA inawapa ushirikiano mkubwa katika kutekeleza mafunzo hayo. “Wataalamu wa TBA wamekuwa msaada mkubwa sana kwetu, wanatufundisha kazi, hali hii inatuongezea ujuzi katika fani zetu”

Pamoja na uhandisi, pia wanafunzi wa kozi zingine ambazo ni uhasibu, manunuzi, ukadiriaji majenzi, ubunifu majengo, sheria na uendelezaji miliki wamepokelewa. Mbali na Chuo kikuu cha Dar es saalam na chuo cha Ardhi, wanafunzi wengine wanatoka vyuo vya CBE, SAUT-MZA, IFM, DIT, Chuo kikuu cha Sayansi na Teknolojia Mbeya (MUSTI) na VETA Dodoma.

Tanzania Census 2022

Mawasiliano yetu

TBA
THE CHIEF EXECUTIVE, TANZANIA BUILDINGS AGENCY (TBA), 13 MOROGORO ROAD, P.O BOX 94, 41102 VIWANDANI, DODOMA TANZANIA, EMAIL: ce@tba.go.tz Website: www.tba.go.tz
Nukushi :
Namba ya Simu : +255 733 483 437, +255 677 108 010
Barua Pepe : barua@tba.go.tz

Linki za Haraka

Linki Linganifu

  • WIZARA YA UJENZI NA UCHUKUZI
  • Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo
  • Utumishi
  • Tume ya Takwimu ya Taifa
  • Tume ya Ajira

©2025 wakala wa majengo tanzania . Haki zote zimehifadhiwa..

Imesanifiwa, Imetengenezwa na Mamlaka ya Serikali Mtandao.Inaendeshwa na Wakala ya Majengo Tanzania