• Maswali
  • Wasiliana Nasi
  • English

Jamhuri ya Muungano wa TanzaniaWakala wa Majengo Tanzania

  • kuhusu Sisi
    • Ujumbe kutoka kwa Mtendaji Mkuu
    • Sisi ni Nani
    • Dira na Dhamira
    • Tunafanya Nini
    • Mikakati
    • Mkataba wa Huduma
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Bodi ya Ushauri
    • Muundo wa Taasisi
    • Senior Management
    • Kurugenzi wa Uwezeshaji wa Huduma
    • Kurugenzi ya Ushauri
    • Kurugenzi ya Ujenzi
    • Kurugenzi ya Miliki
    • Meneja wa Mikoa
  • Nyumba
    • Nyumba za Kuuza
    • Nyumba za Kupangisha
    • Fomu ya Ununuzi wa Nyumba
    • Fomu ya ununuzi wa Nyumba
  • Miradi
    • Miradi Tunayoishikilia
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Iliyo Katika usanifu
    • Miradi Tunayotegemea kufanya
  • Machapisho
    • Machapisho
  • Kituo Cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha
  • Ununuzi
    • Mpango wa Manunuzi wa Mwaka
    • Mialiko ya zabuni
    • Orodha ya Wazabuni Walioshinda

Habari Mpya

  • SERIKALI YAFUNGUA MILANGO YA UWEKEZAJI KWENYE UJENZI WA NYUMBA ZA MAKAZI

    tokea mwezi 1
  • MENEJIMENTI YA TBA YAHIMIZWA KUKUTANA MARA KWA MARA.

    tokea miezi 2
  • TBA YAKUTANA NA WAWEKEZAJI KUTOKA JAPAN.

    tokea miezi 2
  • TBA NA ZBA KUENDELEZA MASHIRIKIANO

    tokea miezi 2

Latest Press Release

TBA YATEKELEZA MIRADI MKOANI MBEYA

Imewekwa: Saturday 28, March 2020

TBA YATEKELEZA MIRADI MKOANI MBEYA

Wakala wa Majengo Tanzania (TBA) umetekeleza miradi mbalimbali Mkoani Mbeya. Miradi iliyotekelezwa inajumuisha miradi ya Ujenzi, Ushauri na ukarabati.

Meneja wa TBA Mkoa wa Mbeya Mhandisi Jafari S. Kiyoga, ameitaja miradi ya ujenzi inayotekelezwa mkoani humo kuwa ni Ujenzi wa jengo la Maktaba ya Chuo cha Sayansi na Teknolojia Mbeya (MUST), Ujenzi wa jengo la Mionzi katika Hospitali ya Rufaa ya kanda Mbeya, Ujenzi wa jengo la upasuaji na jengo la Wodi ya wagonjwa wa Upasuaji katika ya Hospitali ya Rufaa ya Mkoa wa Mbeya.

Pia aliitaja miradi ya ushauri kuwa ni Ujenzi wa jengo la Mahakama ya Mwanzo Uyole, Ujenzi wa jengo la Mahakama ya Wilaya ya Chunya, Ujenzi wa ofisi za bonde la ziwa Rukwa, Ujenzi wa jengo la Mamlaka ya Maji safi na Maji taka Mbeya, na ujenzi wa mgahawa na fensi katika ofisi za TFS za kanda. Vile vile aliutaja Mradi wa ukarabati kuwa ni Maboresho ya jengo la intern kuwa Ward Grade 1 katika Hospitali ya rufaa ya Kanda Mbeya. Vile vile aliutaja mradi unaotarajiwa kuanza hivi karibuni kuwa ni mradi wa ujenzi wa ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Mbeya.

Akiongea juu ya ukarabati wa karakana katika mkoa wake, Meneja wa TBA Mkoa wa Mbeya amesema kuwa pindi ukarabati utakapokamilika watakuwa na uwezo wa kuzalisha samani nyingi za kisasa zitakazotumika kwenye miradi mbalimbali inayotekelezwa katika mikoa ya jirani, kuongeza mapato ya TBA na kutoa nafasi za ajira kwa watanzania.

Akizungumzia juu ya ujenzi wa jengo la Maktaba ya MUST, Makamu Mkuu wa Chuo Prof. Aloyce Mvuma alisema anapongeza jitihada zilizofanywa na TBA katika ujenzi wa jengo hilo ambalo limekamilika kwa asilimia 97 na lina uwezo wa kupokea wanafunzi wengi kwa wakati mmoja kinyume na jengo lililokuwepo hapo awali. Pia Prof. Mvuma alisema Maktaba hiyo imesanifiwa katika muundo wa kipekee kabisa tofauti na maktaba nyingine kwani inauwezo wa kuratibu shughuli nyingi kwa wakati mmoja bila kuwa na muingiliano wowote. Aidha, Prof. Mvuma amepongeza ushirikiano uliooneshwa na ofisi ya TBA Mkoa wa Mbeya kwa kipindi chote cha ujenzi.

Tanzania Census 2022

Mawasiliano yetu

TBA
THE CHIEF EXECUTIVE, TANZANIA BUILDINGS AGENCY (TBA), 13 MOROGORO ROAD, P.O BOX 94, 41102 VIWANDANI, DODOMA TANZANIA, EMAIL: ce@tba.go.tz Website: www.tba.go.tz
Nukushi :
Namba ya Simu : +255 733 483 437, +255 677 108 010
Barua Pepe : barua@tba.go.tz

Linki za Haraka

Linki Linganifu

  • WIZARA YA UJENZI NA UCHUKUZI
  • Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo
  • Utumishi
  • Tume ya Takwimu ya Taifa
  • Tume ya Ajira

©2025 wakala wa majengo tanzania . Haki zote zimehifadhiwa..

Imesanifiwa, Imetengenezwa na Mamlaka ya Serikali Mtandao.Inaendeshwa na Wakala ya Majengo Tanzania