• Maswali
  • Wasiliana Nasi
  • English

Jamhuri ya Muungano wa TanzaniaWakala wa Majengo Tanzania

  • kuhusu Sisi
    • Ujumbe kutoka kwa Mtendaji Mkuu
    • Sisi ni Nani
    • Dira na Dhamira
    • Tunafanya Nini
    • Mikakati
    • Mkataba wa Huduma
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Bodi ya Ushauri
    • Muundo wa Taasisi
    • Senior Management
    • Kurugenzi wa Uwezeshaji wa Huduma
    • Kurugenzi ya Ushauri
    • Kurugenzi ya Ujenzi
    • Kurugenzi ya Miliki
    • Meneja wa Mikoa
  • Nyumba
    • Nyumba za Kuuza
    • Nyumba za Kupangisha
    • Fomu ya Ununuzi wa Nyumba
    • Fomu ya ununuzi wa Nyumba
  • Miradi
    • Miradi Tunayoishikilia
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Iliyo Katika usanifu
    • Miradi Tunayotegemea kufanya
  • Machapisho
    • Machapisho
  • Kituo Cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha
  • Ununuzi
    • Mpango wa Manunuzi wa Mwaka
    • Mialiko ya zabuni
    • Orodha ya Wazabuni Walioshinda

Habari Mpya

  • SERIKALI YAFUNGUA MILANGO YA UWEKEZAJI KWENYE UJENZI WA NYUMBA ZA MAKAZI

    tokea mwezi 1
  • MENEJIMENTI YA TBA YAHIMIZWA KUKUTANA MARA KWA MARA.

    tokea mwezi 1
  • TBA YAKUTANA NA WAWEKEZAJI KUTOKA JAPAN.

    tokea mwezi 1
  • TBA NA ZBA KUENDELEZA MASHIRIKIANO

    tokea mwezi 1

Latest Press Release

KAMATI YA BUNGE YAITAKA WIZARA YA UJENZI KUISAIDIA TBA.

Imewekwa: Thursday 23, March 2023

Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu ikiongozwa na Mwenyekiti wake Mhe. Selemani Kakoso (Mb) imefanya ziara ya kutembelea na kukagua maendeleo ya utekelezaji wa mradi wa ujenzi wa nyumba za makazi ya watumishi wa umma katika eneo la Temeke Kota jijini Dar es Salaam.

Akizungumza katika ziara hiyo Mhe. Kakoso amesema TBA imekuwa ikifanya kazi kubwa katika utekelezaji wa miradi mbalimbali ya ujenzi wa nyumba za makazi hususani mradi wa ujenzi wa Temeke Kota. Amesema kuwa ni vyema Wizara ikasaidia upatikanaji wa fedha kwa wakati ili mradi huo uweze kutekelezwa kwa wakati uliokusudiwa.

Aidha, Mhe. Kakoso amesema ni wakati sahihi sasa TBA kuanza kujiendesha kibiashara kwa kushirikiana na Sekta Binafsi na kuacha kutegemea fedha za ruzuku kutoka Serikalini kutekeleza miradi yake.

Pia Mhe. Kakoso ameitaka Wizara ya ujenzi kuisaidia TBA kudai madeni kutoka taasisi mbalimbali za Serikali. "TBA inapitia kipindi kigumu kwasababu ya kuwa na malimbikizo makubwa ya madeni kutoka taasisi mbalimbali hivyo ni vyema Wizara ya Ujenzi mkaisaidia ili fedha hizo ziende kufanya uwekezaji mkubwa zaidi" amesema Mhe. Kakoso.

Naye, Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi Mhe. Prof. Makame Mbarawa (Mb) amesema amepokea maelekezo yote yaliyotolewa na Kamati ya Miundombinu na kuahidi kwenda kuyafanyia kazi. Pia Mhe. Mbarawa ameipongeza TBA kwa hatua inazochukua kuwaondoa wadaiwa sugu na kuwaelekeza wapangaji wa nyumba za TBA kulipa kodi ya pango kwa wakati vinginevyo wataondolewa katika nyumba hizo kama ambavyo zoezi la kuwaondoa linavyoendelea.

Kwa upande wake Mtendaji Mkuu wa TBA Arch. Daud Kondoro ameishukuru Kamati kwa kufanya ziara hiyo na kuahidi kuyafanyia kazi maelekezo na mapendekezo yote yaliyotolewa.

Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Miundombinu imefanya ziara ya katika mradi wa Ujenzi wa nyumba za watumishi wa Umma unaotekelezwa na TBA kama Mkandarasi na Mshauri Elekezi katika eneo la Temeke Kota.

Tanzania Census 2022

Mawasiliano yetu

TBA
THE CHIEF EXECUTIVE, TANZANIA BUILDINGS AGENCY (TBA), 13 MOROGORO ROAD, P.O BOX 94, 41102 VIWANDANI, DODOMA TANZANIA, EMAIL: ce@tba.go.tz Website: www.tba.go.tz
Nukushi :
Namba ya Simu : +255 733 483 437, +255 677 108 010
Barua Pepe : barua@tba.go.tz

Linki za Haraka

Linki Linganifu

  • WIZARA YA UJENZI NA UCHUKUZI
  • Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo
  • Utumishi
  • Tume ya Takwimu ya Taifa
  • Tume ya Ajira

©2025 wakala wa majengo tanzania . Haki zote zimehifadhiwa..

Imesanifiwa, Imetengenezwa na Mamlaka ya Serikali Mtandao.Inaendeshwa na Wakala ya Majengo Tanzania