• Maswali
  • Wasiliana Nasi
  • English

Jamhuri ya Muungano wa TanzaniaWakala wa Majengo Tanzania

  • kuhusu Sisi
    • Ujumbe kutoka kwa Mtendaji Mkuu
    • Sisi ni Nani
    • Dira na Dhamira
    • Tunafanya Nini
    • Mikakati
    • Mkataba wa Huduma
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Bodi ya Ushauri
    • Muundo wa Taasisi
    • Senior Management
    • Kurugenzi wa Uwezeshaji wa Huduma
    • Kurugenzi ya Ushauri
    • Kurugenzi ya Ujenzi
    • Kurugenzi ya Miliki
    • Meneja wa Mikoa
  • Nyumba
    • Nyumba za Kuuza
    • Nyumba za Kupangisha
    • Fomu ya Ununuzi wa Nyumba
    • Fomu ya ununuzi wa Nyumba
  • Miradi
    • Miradi Tunayoishikilia
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Iliyo Katika usanifu
    • Miradi Tunayotegemea kufanya
  • Machapisho
    • Machapisho
  • Kituo Cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha
  • Ununuzi
    • Mpango wa Manunuzi wa Mwaka
    • Mialiko ya zabuni
    • Orodha ya Wazabuni Walioshinda

Habari Mpya

  • SERIKALI YAFUNGUA MILANGO YA UWEKEZAJI KWENYE UJENZI WA NYUMBA ZA MAKAZI

    tokea mwezi 1
  • MENEJIMENTI YA TBA YAHIMIZWA KUKUTANA MARA KWA MARA.

    tokea mwezi 1
  • TBA YAKUTANA NA WAWEKEZAJI KUTOKA JAPAN.

    tokea mwezi 1
  • TBA NA ZBA KUENDELEZA MASHIRIKIANO

    tokea mwezi 1

Latest Press Release

MAKAMU WA RAIS DKT. MPANGO AZINDUA RASMI JENGO LA TBA JIJINI ARUSHA

Imewekwa: Sunday 06, August 2023

Makamu wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. Philip Mpango ameupongeza kwa Wakala wa Majengo Tanzania (TBA) kwa kufanikisha kukamilisha ujenzi wa jengo la kisasa la makazi kwa kuzingatia ubora, tija, gharama nafuu pamoja na kuwa na huduma kisasa zinazoendana na mahitaji ya teknolojia.

Makamu wa Rais amesema hayo leo tarehe 04 Agosti 2023 wakati wa Hafla ya Ufunguzi wa Jengo la makazi la Kibiashara lililopo eneo la Sekei jijini Arusha ambalo limejengwa na Wakala wa Majengo Tanzania (TBA)

Ameongeza kwamba ni vyema TBA ikafanya mapinduzi makubwa ya kiutendaji, kuongeza ubunifu na kujenga misingi mizuri ya kujiendesha kibiashara ili kuweza kupata mapato zaidi na kujiendesha pasipo kutegemea ruzuku kutoka serikalini.

Halikadhalika Makamu wa Rais amewataka TBA kuweka utaratibu shirikishi kwa lengo la kuimarisha ulinzi na usalama wa watu na mali zao katika maeneo ya nyumba hizo. Pia amewasihi wapangaji watakaopanga kwenye nyumba hizo kuzitunza na kuhakikisha zinabaki katika hali ya ubora wake ikiwemo kuzingatia masuala ya usafi na utunzaji wa mazingira.

Makamu wa Rais amesema uwekezaji katika Sekta ya ujenzi ni miongoni mwa vipaumbele muhimu vya Serikali ya Awamu ya Sita ambayo inaendelea kuhakikisha miradi hiyo inatekelezwa kama ilivyopangwa. Aidha amesema Serikali itaendelea kuunga mkono ubunifu na mipango ya Taasisi kama TBA kuwa na miradi mingi zaidi ya ujenzi ili kuongeza makusanyo ya ndani na kupunguza utegemezi wa ruzuku kutoka Serikalini.

Naye Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi Profesa Makame Mbarawa amesema kukamilika kwa jengo hilo kutasaidia upatikanaji wa makazi ya uhakika kwa wakaazi waliopo jijini Arusha.

Profesa Mbarawa ameongeza kwamba ujenzi wa mradi huo umesaidia Wataalamu wazawa wa fani za ujenzi kujengewa uwezo wa taaluma kwa vitendo pamoja na kusaidia kuendelea kukua kwa kasi kwa jiji la Arusha lililopangwa vizuri kwa kuzingatia mipango miji, kuongezeka kwa mapato ya serikali na huduma za kijamii katika jiji hilo.

Awali akitoa taarifa ya utekelezaji wa mradi huo, Mtendaji Mkuu wa TBA Arch. Daud Kondoro amesema jengo hilo la makazi lina sakafu 12 ikijumuisha sakafu moja iliyo chini ya usawa wa ardhi (basement) itakayotumika kama sehemu ya kuhifadhia (storage). Katika sakafu 11 zilizobaki, kila sakafu ina nyumba (apartments) mbili (2) na hivyo kulifanya jengo hili kuwa na uwezo wa kuchukua jumla ya familia 22.

Kandoro amesema TBA inaendelea kutekeleza miradi mingine nchi nzima kwa fedha za ruzuku na makusanyo ya ndani ikiwemo mradi wa ujenzi wa nyumba mpya 20 za Viongozi katika eneo la Kisasa Dodoma, ukamilishaji wa nyumba za majaji kwenye Mikoa ya Kilimanjaro, Mtwara, Shinyanga, Tabora na Kagera, ukarabati wa nyumba za makazi ya watumishi wa Umma na Viongozi Tanzania Bara ili kuwawezesha kuishi katika mazingira bora, Ujenzi wa nyumba za makazi kwa Watumishi wa Umma katika eneo la Magomeni Kota na Temeke Kota, Ujenzi wa jengo la makazi eneo la Masaki,pamoja na ujenzi wa nyumba 13 za watumishi Mikoani.

Tanzania Census 2022

Mawasiliano yetu

TBA
THE CHIEF EXECUTIVE, TANZANIA BUILDINGS AGENCY (TBA), 13 MOROGORO ROAD, P.O BOX 94, 41102 VIWANDANI, DODOMA TANZANIA, EMAIL: ce@tba.go.tz Website: www.tba.go.tz
Nukushi :
Namba ya Simu : +255 733 483 437, +255 677 108 010
Barua Pepe : barua@tba.go.tz

Linki za Haraka

Linki Linganifu

  • WIZARA YA UJENZI NA UCHUKUZI
  • Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo
  • Utumishi
  • Tume ya Takwimu ya Taifa
  • Tume ya Ajira

©2025 wakala wa majengo tanzania . Haki zote zimehifadhiwa..

Imesanifiwa, Imetengenezwa na Mamlaka ya Serikali Mtandao.Inaendeshwa na Wakala ya Majengo Tanzania