• Maswali
  • Wasiliana Nasi
  • English

Jamhuri ya Muungano wa TanzaniaWakala wa Majengo Tanzania

  • kuhusu Sisi
    • Ujumbe kutoka kwa Mtendaji Mkuu
    • Sisi ni Nani
    • Dira na Dhamira
    • Tunafanya Nini
    • Mikakati
    • Mkataba wa Huduma
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Bodi ya Ushauri
    • Muundo wa Taasisi
    • Senior Management
    • Kurugenzi wa Uwezeshaji wa Huduma
    • Kurugenzi ya Ushauri
    • Kurugenzi ya Ujenzi
    • Kurugenzi ya Miliki
    • Meneja wa Mikoa
  • Nyumba
    • Nyumba za Kuuza
    • Nyumba za Kupangisha
    • Fomu ya Ununuzi wa Nyumba
    • Fomu ya ununuzi wa Nyumba
  • Miradi
    • Miradi Tunayoishikilia
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Iliyo Katika usanifu
    • Miradi Tunayotegemea kufanya
  • Machapisho
    • Machapisho
  • Kituo Cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha
  • Ununuzi
    • Mpango wa Manunuzi wa Mwaka
    • Mialiko ya zabuni
    • Orodha ya Wazabuni Walioshinda

Habari Mpya

  • SERIKALI YAFUNGUA MILANGO YA UWEKEZAJI KWENYE UJENZI WA NYUMBA ZA MAKAZI

    tokea mwezi 1
  • MENEJIMENTI YA TBA YAHIMIZWA KUKUTANA MARA KWA MARA.

    tokea miezi 2
  • TBA YAKUTANA NA WAWEKEZAJI KUTOKA JAPAN.

    tokea miezi 2
  • TBA NA ZBA KUENDELEZA MASHIRIKIANO

    tokea miezi 2

Latest Press Release

WANAWAKE TBA WASHIRIKI MAADHIMISHO YA SIKU YA WANAWAKE DUNIANI

Imewekwa: Monday 09, March 2020

Wanawake wa Wakala wa Majengo Tanzania (TBA) walipata fursa ya kushiriki maadhimisho ya siku ya wanawake duniani Machi 8, 2020 katika maeneo mbalimbali nchini yenye kauli mbiu “Kizazi cha Usawa kwa Maendeleo ya Tanzania ya sasa na baadaye”. Pia walipata nafasi ya kutembelea Hospitali ya Amana jijini Dar es Salaam na kutembelea Kituo cha watoto yatima cha TCRC kilichopo Nyansaka jijini Mwanza.

Katika Mkoa wa Dar es Salaam kongamano la maadhimisho ya siku ya wanawake lilifanyika katika viwanja vya Leaders, Kinondoni ambapo Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Mhe. Paul Makonda alikuwa mgeni rasmi. Katika hotuba yake, Mkuu wa Mkoa alisema hataki kumwona mwanamke yeyote katika mkoa anaouongoza akinyanyasika, ndio maana aliamua kuwasaidia wanawake waliotelekezwa na wenza wao na kutoa namba za mawasiliano ambayo wanaweza kupiga bure.

Aidha, katika Mkoa wa Mwanza wanawake wa TBA walishiriki maadhimisho siku ya wanawake duniani katika viwanja vya Furahisha ambapo Mgeni rasmi alikuwa Mkuu wa Wilaya ya Nyamagama Mhe. Dkt. Philis M. Nyimbi ambaye alisisitiza umuhimu wa wanawake kupewa mikopo, kupewa kipaumbele katika nyanja mbalimbali pamoja na kuthubutu kushiriki katika vinyang’anyiro vya kugombea nafasi mbalimbali za Uongozi bila kusubiri upendeleo wa viti maalum.

Katika kuadhimisha siku ya wanawake duniani, wanawake wa TBA walipata nafasi ya kutembelea Hospitali ya Amana jijini Dar es Salaam na kutoa vifaa tiba pamoja na mashuka kwa mama wajawazito. Vile vile Mkoani Mwanza wanawake wa TBA walitembelea kituo cha watoto yatima cha TCRC kilichopo Nyansaka na kutoa mahitaji mbalimbali yakiwemo mahindi gunia 3, sukari kilo 25, sabuni ya unga, mchele kilo 100, taulo za kike pamoja na mahitaji mengine ya msingi.

Tanzania Census 2022

Mawasiliano yetu

TBA
THE CHIEF EXECUTIVE, TANZANIA BUILDINGS AGENCY (TBA), 13 MOROGORO ROAD, P.O BOX 94, 41102 VIWANDANI, DODOMA TANZANIA, EMAIL: ce@tba.go.tz Website: www.tba.go.tz
Nukushi :
Namba ya Simu : +255 733 483 437, +255 677 108 010
Barua Pepe : barua@tba.go.tz

Linki za Haraka

Linki Linganifu

  • WIZARA YA UJENZI NA UCHUKUZI
  • Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo
  • Utumishi
  • Tume ya Takwimu ya Taifa
  • Tume ya Ajira

©2025 wakala wa majengo tanzania . Haki zote zimehifadhiwa..

Imesanifiwa, Imetengenezwa na Mamlaka ya Serikali Mtandao.Inaendeshwa na Wakala ya Majengo Tanzania