• Maswali
  • Wasiliana Nasi
  • English

Jamhuri ya Muungano wa TanzaniaWakala wa Majengo Tanzania

  • kuhusu Sisi
    • Ujumbe kutoka kwa Mtendaji Mkuu
    • Sisi ni Nani
    • Dira na Dhamira
    • Tunafanya Nini
    • Mikakati
    • Mkataba wa Huduma
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Bodi ya Ushauri
    • Muundo wa Taasisi
    • Senior Management
    • Kurugenzi wa Uwezeshaji wa Huduma
    • Kurugenzi ya Ushauri
    • Kurugenzi ya Ujenzi
    • Kurugenzi ya Miliki
    • Meneja wa Mikoa
  • Nyumba
    • Nyumba za Kuuza
    • Nyumba za Kupangisha
    • Fomu ya Ununuzi wa Nyumba
    • Fomu ya ununuzi wa Nyumba
  • Miradi
    • Miradi Tunayoishikilia
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Iliyo Katika usanifu
    • Miradi Tunayotegemea kufanya
  • Machapisho
    • Machapisho
  • Kituo Cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha
  • Ununuzi
    • Mpango wa Manunuzi wa Mwaka
    • Mialiko ya zabuni
    • Orodha ya Wazabuni Walioshinda

Habari Mpya

  • SERIKALI YAFUNGUA MILANGO YA UWEKEZAJI KWENYE UJENZI WA NYUMBA ZA MAKAZI

    tokea mwezi 1
  • MENEJIMENTI YA TBA YAHIMIZWA KUKUTANA MARA KWA MARA.

    tokea miezi 2
  • TBA YAKUTANA NA WAWEKEZAJI KUTOKA JAPAN.

    tokea miezi 2
  • TBA NA ZBA KUENDELEZA MASHIRIKIANO

    tokea miezi 2

Latest Press Release

TBA itaendelea kuwa Taasisi imara kutekeleza Miradi kwa ubora

Imewekwa: Saturday 04, April 2020

Wakala wa Majengo Tanzania (TBA) utaendelea kuwa Wakala bora kwa kutumia wataalam iliyonao kutekeleza miradi ya Serikali kwa weledi na kuzingatia ubora.

“Siri kubwa ya kukamilika kwa Miradi ni kutokana na kupata fedha kwa wakati”

Mtendaji Mkuu wa TBA, Arch. Daudi Kondoro amebainisha hayo akijibu swali la Mwandishi wa Gazeti la Serikali la Daily News katika mahojiano maalumu yaliyofanyika Jijini Dodoma hivi karibuni.

“Sisi kama TBA kwa kawaida hatuwezi kwenda hatua nyingine ya ujenzi bila ya kujiridhisha hatua tuliyomaliza kama ipo sahihi, hasa kwa kuangalia mahitaji yaliyohitajika katika hatua hiyo” amesisitiza Arch. Kondoro

Arch. Kondoro, ameitaja miradi ya Wilaya ya Kigamboni ambayo ni ujenzi wa Ofisi za Mkuu wa Wilaya na Mkurugenzi wa Manispaa zilizokamilika hivi karibuni na kukabidhiwa kwa wakati, kuwa ni kielelezo tosha cha ubora, weledi na gharama nafuu, hali inayochangiwa na upatikanaji wa fedha kwa wakati.

Ameeleza kuwa baadhi ya miradi mikubwa ya Kitaifa ambayo TBA inasimamia ni pamoja na ujenzi wa Rada katika Kiwanja cha ndege cha Kimataifa cha Julius Nyerere (JNIA), Kiwanja cha ndege cha Kimataifa cha Kilimanjaro (KIA), Kiwanja cha ndege cha Kimataifa cha Songwe na kiwanja cha ndege cha Mwanza, ujenzi wa Kituo cha pamoja cha forodha kinachojengwa katika mpaka wa Tanzania na Malawi eneo la Kasumulu , Mkoani Mbeya na mradi wa ujenzi wa Maghala ya kuhifadhi chakula maarufu kama Vihenge ambao unatekelezwa katika mikoa nane ya Dodoma, Katavi, Ruvuma, Njombe, Songwe, Rukwa, Shinyanga na Manyara.

“Mradi wa ujenzi wa maghala ya kuhifadhia chakula, umefikia asilimia 80 kukamilika, mradi huu ni wa Kitaifa ambao unatekelezwa katika mikoa 8. Tuna matumaini mradi huu ukikamilika utakuwa ni msaada mkubwa katika uhifadhi wa chakula nchini”

Kwa upande wa vifaa, Mtendaji Mkuu amefafanua kuwa TBA ina mitambo miwili (2) ya kuchakata zege, mmoja umefungwa Dar es Saalam katika mradi wa Magomeni Kota na mwingine upo Nzuguni mkoani Dodoma. Pia TBA ina kiwanda cha kutengeneza tofali ambacho kipo Magomeni. Ametaja faida ya kiwanda hicho kuwa kinauwezo wa kutengeneza tofali zaidi ya 2000 kwa siku, na matofali hayo yanatumika katika ujenzi wa nyumba za Magomeni Kota, hivyo kimesaidia kupunguza gharama.

Naye Mkurugenzi wa Ushauri Arch. Wenceslaus Kizaba akizungumzia ujenzi wa Mji wa Serikali amesema, michoro ya majengo kwa awamu ya pili imekamilika na kupitishwa na Mamlaka husika tayari kwa utekelezaji unaofuata ambao ni ujenzi.

Ujenzi wa mji wa Serikali awamu ya pili utabadilisha muonekano wa mandhari yaliyopo kwa sasa, kwa kuwa na majengo ya ghorofa, barabara za lami na mazingira yenye kuvutia.

Wakala wa Majengo Tanzania (TBA) ni taasisi ya Serikali iliyoanzishwa mwaka 2002 kwa lengo la kusimamia miliki za Serikali.

Tanzania Census 2022

Mawasiliano yetu

TBA
THE CHIEF EXECUTIVE, TANZANIA BUILDINGS AGENCY (TBA), 13 MOROGORO ROAD, P.O BOX 94, 41102 VIWANDANI, DODOMA TANZANIA, EMAIL: ce@tba.go.tz Website: www.tba.go.tz
Nukushi :
Namba ya Simu : +255 733 483 437, +255 677 108 010
Barua Pepe : barua@tba.go.tz

Linki za Haraka

Linki Linganifu

  • WIZARA YA UJENZI NA UCHUKUZI
  • Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo
  • Utumishi
  • Tume ya Takwimu ya Taifa
  • Tume ya Ajira

©2025 wakala wa majengo tanzania . Haki zote zimehifadhiwa..

Imesanifiwa, Imetengenezwa na Mamlaka ya Serikali Mtandao.Inaendeshwa na Wakala ya Majengo Tanzania