• Maswali
  • Wasiliana Nasi
  • English

Jamhuri ya Muungano wa TanzaniaWakala wa Majengo Tanzania

  • kuhusu Sisi
    • Ujumbe kutoka kwa Mtendaji Mkuu
    • Sisi ni Nani
    • Dira na Dhamira
    • Tunafanya Nini
    • Mikakati
    • Mkataba wa Huduma
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Bodi ya Ushauri
    • Muundo wa Taasisi
    • Senior Management
    • Kurugenzi wa Uwezeshaji wa Huduma
    • Kurugenzi ya Ushauri
    • Kurugenzi ya Ujenzi
    • Kurugenzi ya Miliki
    • Meneja wa Mikoa
  • Nyumba
    • Nyumba za Kuuza
    • Nyumba za Kupangisha
    • Fomu ya Ununuzi wa Nyumba
    • Fomu ya ununuzi wa Nyumba
  • Miradi
    • Miradi Tunayoishikilia
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Iliyo Katika usanifu
    • Miradi Tunayotegemea kufanya
  • Machapisho
    • Machapisho
  • Kituo Cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha
  • Ununuzi
    • Mpango wa Manunuzi wa Mwaka
    • Mialiko ya zabuni
    • Orodha ya Wazabuni Walioshinda

Habari Mpya

  • SERIKALI YAFUNGUA MILANGO YA UWEKEZAJI KWENYE UJENZI WA NYUMBA ZA MAKAZI

    tokea siku 3
  • MENEJIMENTI YA TBA YAHIMIZWA KUKUTANA MARA KWA MARA.

    tokea wiki 3
  • TBA YAKUTANA NA WAWEKEZAJI KUTOKA JAPAN.

    tokea wiki 3
  • TBA NA ZBA KUENDELEZA MASHIRIKIANO

    tokea wiki 3

Latest Press Release

MKUU WA WILAYA YA KINONDONI ARIDHISHWA NA MAENDELEO YA UJENZI WA MRADI WA MAGOMENI KOTA

Imewekwa: Thursday 03, October 2019

Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni Mhe. Daniel Chongolo atembelea mradi wa ujenzi wa nyumba za makazi ya wananchi Magomeni kota uliosanifiwa na kujengwa na Wakala wa Majengo Tanzania (TBA) na kuridhishwa na kasi ya ujenzi wa mradi huo unaotarajiwa kukamilika mnamo mwezi Desemba mwaka huu.

Katika ziara yake Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni alitembelea majengo ya magorofa yanayojengwa, kiwanda kidogo cha kufyatua tofali pamoja na mtambo wa kuchakata zege (Batching Plant) na kujionea namna ambavyo TBA unatumia kikosi chake maalum cha ujenzi (TBA Brigade) katika kupunguza gharama za ujenzi. Vile vile uwepo wa viwanda hivi vidogo unapunguza gharama za mradi kwa kuwa malighafi nyingi za ujenzi zinazalishwa na TBA na kuepuka kununua kutoka kwa wazabuni ambao bei zao zipo juu.

Akizungumza wakati wa ziara, Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni amesema “Napenda kuchukua fursa hii kuwapongeza TBA kwa kuwa wazalendo na kuamua kutumia kikosi kazi chake cha ujenzi katika kuandaa tofali na kuchakata zege ili kupunguza gharama za mradi na pia kwa kuwatumia vijana wa maeneo jirani na mradi kama vibarua na mama lishe katika kutoa huduma kwenye eneo la mradi kwani hiyo imetoa fursa kwa wakazi wa wilaya ya Kinondoni kujipatia kipato”

Akiuelezea mradi huo Meneja wa mradi kutoka TBA Mbunifu Majengo Bernard Mayemba amesema “Mradi huo unatarajiwa kukamilika ifikapo mwezi Desemba mwaka huu endapo hapatatokea changamoto zozote za kiutendaji”. Mradi huu unategemewa kuchukua jumla ya kaya 656 ikiwa ni utekelezaji wa agizo la Mhe. Rais Dkt. John Pombe Magufuli la kujenga kaya 644. TBA inachukua jitihada za haraka kuukamilisha mradi huu kwa kufanya kazi usiku na mchana ili kufikia malengo hayo.

Tanzania Census 2022

Mawasiliano yetu

TBA
THE CHIEF EXECUTIVE, TANZANIA BUILDINGS AGENCY (TBA), 13 MOROGORO ROAD, P.O BOX 94, 41102 VIWANDANI, DODOMA TANZANIA, EMAIL: ce@tba.go.tz Website: www.tba.go.tz
Nukushi :
Namba ya Simu : +255 733 483 437, +255 677 108 010
Barua Pepe : barua@tba.go.tz

Linki za Haraka

Linki Linganifu

  • WIZARA YA UJENZI NA UCHUKUZI
  • Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo
  • Utumishi
  • Tume ya Takwimu ya Taifa
  • Tume ya Ajira

©2025 wakala wa majengo tanzania . Haki zote zimehifadhiwa..

Imesanifiwa, Imetengenezwa na Mamlaka ya Serikali Mtandao.Inaendeshwa na Wakala ya Majengo Tanzania