• Maswali
  • Wasiliana Nasi
  • English

Jamhuri ya Muungano wa TanzaniaWakala wa Majengo Tanzania

  • kuhusu Sisi
    • Ujumbe kutoka kwa Mtendaji Mkuu
    • Sisi ni Nani
    • Dira na Dhamira
    • Tunafanya Nini
    • Mikakati
    • Mkataba wa Huduma
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Bodi ya Ushauri
    • Muundo wa Taasisi
    • Senior Management
    • Kurugenzi wa Uwezeshaji wa Huduma
    • Kurugenzi ya Ushauri
    • Kurugenzi ya Ujenzi
    • Kurugenzi ya Miliki
    • Meneja wa Mikoa
  • Nyumba
    • Nyumba za Kuuza
    • Nyumba za Kupangisha
    • Fomu ya Ununuzi wa Nyumba
    • Fomu ya ununuzi wa Nyumba
  • Miradi
    • Miradi Tunayoishikilia
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Iliyo Katika usanifu
    • Miradi Tunayotegemea kufanya
  • Machapisho
    • Machapisho
  • Kituo Cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha
  • Ununuzi
    • Mpango wa Manunuzi wa Mwaka
    • Mialiko ya zabuni
    • Orodha ya Wazabuni Walioshinda

Habari Mpya

  • SERIKALI YAFUNGUA MILANGO YA UWEKEZAJI KWENYE UJENZI WA NYUMBA ZA MAKAZI

    tokea mwezi 1
  • MENEJIMENTI YA TBA YAHIMIZWA KUKUTANA MARA KWA MARA.

    tokea miezi 2
  • TBA YAKUTANA NA WAWEKEZAJI KUTOKA JAPAN.

    tokea miezi 2
  • TBA NA ZBA KUENDELEZA MASHIRIKIANO

    tokea miezi 2

Latest Press Release

KATIBU MKUU WIZARA YA UJENZI ARCH. ELIUS MWAKALINGA ATEMBELEA NA KUKAGUA MAENDELEO YA MRADI WA MAGOMENI KOTA

Imewekwa: Thursday 22, October 2020

Katibu Mkuu Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano (Ujenzi) Arch. Elius Mwakalinga leo Oktoba 20, 2020 ametembelea na kukagua maendeleo ya mradi wa Ujenzi wa nyumba za makazi ya wananchi Magomeni Kota jijini Dar es Salaam. Mradi huo unatarajiwa kutoa makazi kwa kaya takribani 656 ambazo zitaishi katika eneo hilo.

Baada ya kutembelea mradi huo Katibu Mkuu amewapongeza na kuwashukuru Wakala wa Majengo Tanzania (TBA) ambao ni wakandarasi na wasimamizi wa mradi huo kwa hatua nzuri ya maendeleo ambayo mradi huo umefikia. Hata hivyo, Katibu Mkuu amesema Serikali kupitia Wizara ya Ujenzi imewapatia TBA kiasi cha shilingi bilioni 9 ili ziweze kusaidia kukamilika kwa mradi huo unaotarajiwa kukamilika Januari 2021.

Aidha, Arch. Elius Mwakalinga amesema mradi huo utakuwa na miundombinu wezeshi kwa wakazi wa eneo hilo Kutokana na uwepo wa huduma mbalimbali za kijamii katika eneo la mradi kama vile Masoko, Maduka, Maeneo ya kupumzika, Sehemu za kufulia pamoja na uwepo wa vifaa vya kujikinga na janga la moto. Akizungumza katika ziara hiyo Arch. Elius Mwakalinga ameipongeza serikali ya awamu ya tano kwa kuwajali wananchi wake na kuweza kufanikisha maendeleo ya Ujenzi wa mradi huo wa Magomeni Kota.

Vilevile, Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Majengo Tanzania (TBA) Arch. Daud W. Kondoro amesema ujenzi huo mpaka sasa umekamilika kwa asilimia themanini na moja (81%) hivyo mpango mkakati wa TBA kwa sasa ni kufanya kazi usiku na mchana ili kukamilisha mradi huo ifikapo Januari 2021.

Pia, Mtendaji Mkuu amesema mradi huo haukuathiriwa na ugonjwa wa Corona kwa kuwa vifaa vingi vya Ujenzi vinanunuliwa ndani ya nchi.

Mradi wa nyumba za makazi Magomeni kota unatekelezwa ikiwa ni ahadi ya Rais wa awamu ya tano wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe. Dkt. John Pombe Magufuli.

Tanzania Census 2022

Mawasiliano yetu

TBA
THE CHIEF EXECUTIVE, TANZANIA BUILDINGS AGENCY (TBA), 13 MOROGORO ROAD, P.O BOX 94, 41102 VIWANDANI, DODOMA TANZANIA, EMAIL: ce@tba.go.tz Website: www.tba.go.tz
Nukushi :
Namba ya Simu : +255 733 483 437, +255 677 108 010
Barua Pepe : barua@tba.go.tz

Linki za Haraka

Linki Linganifu

  • WIZARA YA UJENZI NA UCHUKUZI
  • Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo
  • Utumishi
  • Tume ya Takwimu ya Taifa
  • Tume ya Ajira

©2025 wakala wa majengo tanzania . Haki zote zimehifadhiwa..

Imesanifiwa, Imetengenezwa na Mamlaka ya Serikali Mtandao.Inaendeshwa na Wakala ya Majengo Tanzania