• Maswali
  • Wasiliana Nasi
  • English

Jamhuri ya Muungano wa TanzaniaWakala wa Majengo Tanzania

  • kuhusu Sisi
    • Ujumbe kutoka kwa Mtendaji Mkuu
    • Sisi ni Nani
    • Dira na Dhamira
    • Tunafanya Nini
    • Mikakati
    • Mkataba wa Huduma
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Bodi ya Ushauri
    • Muundo wa Taasisi
    • Senior Management
    • Kurugenzi wa Uwezeshaji wa Huduma
    • Kurugenzi ya Ushauri
    • Kurugenzi ya Ujenzi
    • Kurugenzi ya Miliki
    • Meneja wa Mikoa
  • Nyumba
    • Nyumba za Kuuza
    • Nyumba za Kupangisha
    • Fomu ya Ununuzi wa Nyumba
    • Fomu ya ununuzi wa Nyumba
  • Miradi
    • Miradi Tunayoishikilia
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Iliyo Katika usanifu
    • Miradi Tunayotegemea kufanya
  • Machapisho
    • Machapisho
  • Kituo Cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha
  • Ununuzi
    • Mpango wa Manunuzi wa Mwaka
    • Mialiko ya zabuni
    • Orodha ya Wazabuni Walioshinda

Habari Mpya

  • SERIKALI YAFUNGUA MILANGO YA UWEKEZAJI KWENYE UJENZI WA NYUMBA ZA MAKAZI

    tokea mwezi 1
  • MENEJIMENTI YA TBA YAHIMIZWA KUKUTANA MARA KWA MARA.

    tokea mwezi 1
  • TBA YAKUTANA NA WAWEKEZAJI KUTOKA JAPAN.

    tokea mwezi 1
  • TBA NA ZBA KUENDELEZA MASHIRIKIANO

    tokea mwezi 1

Latest Press Release

WAZIRI MHE. SIMBACHAWENE AZITAKA TAASISI ZA UMMA KUZINGATIA MIKATABA YA HUDUMA KWA MTEJA KATIKA KUTOA HUDUMA BORA.

Imewekwa: Monday 26, June 2023

Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma na Utawala Bora, Mhe. George Simbachawene amewataka Watumishi wa Umma kutoa huduma bora kwa wananchi huku akizitaka Taasisi zote za Umma kuhuisha Mikataba ya Huduma kwa Mteja kwani ni nyenzo na kiungo muhimu katika kuboresha utendaji kazi kati ya Serikali na Wananchi inaowahudumia.

Ametoa kauli hiyo leo Ijumaa Juni 23, 2023 wakati akizungumza na watumishi mbalimbali wa Serikali pamoja na wananchi walioshirikikwenye Uzinduziwa Mikataba ya Hudumakwa Mteja ya Taasisi za Umma katikaKilele cha Maadhimisho ya Wiki yaUtumishi wa Umma ambayo kitaifa yamefanyika katika Viwanja vya Nyerere Square Jijini Dodoma.

Mhe. Simbachawene amewataka Watumishi hao kutambua kuwa wanapotoa huduma bora kwa wananchi wanamuwakilisha Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan ambaye amekuwa akisisitiza suala hilo mara kwa mara.

Kufuatia hatua hiyo, amezitaka Taasisi za Umma kuzingatia Mikataba ya Huduma kwa Mteja katika utoaji wa huduma kwa wananchi ili haki na wajibu wa pande zote mbili utendeke kwa watoa huduma na wapokea huduma ambao ndio wateja. Ameongeza kuwa Ofisi yake ina wajibu wa kusimamia mifumo na viwango vya utendaji kazi Serikalini kwa lengo la kuongeza uwajibikaji na kuboresha utoaji wa huduma kwa wananchi na moja ya mifumo na viwangovya Utendaji Kazi huo ni Mkataba wa Huduma kwa Mteja.

Awali, Katibu Mkuu Ofisi ya Rais Menejimenti ya Utumishi wa Umma, Bw. Juma Mkomi amesema uzinduzi wa Mikataba ya Huduma kwa Mteja ni moja ya hatua muhimu ya kuboresha huduma bora kwa wananchi ambapo amesema jumla ya Mikataba ya Huduma kwa Mteja Taasisi za Umma imeweza kuzinduliwa."Uzinduzi wa mikataba hii ya Huduma kwa mteja inakwenda kuwezesha watumishi wa umma kuwa na utamaduni wa utendaji kazi unaojali matokeo na tija kwa wakati" amesema Mkomi

Aidha, Katibu Mkuu Mkomi ametumia fursa hiyo kuzipongeza Taasisi za Umma ambazo zimeadhimisha Wiki ya Utumishi wa Umma kwenye maeneo yao kama ilivyoelekezwa na Ofisi yake.

Naye, Mtendaji Mkuu wa Wakala wa Majengo Tanzania (TBA) Arch. Daudi Kandoro akitoa neno la shukrani mara baada ya uzinduzi wa mikataba hiyokwa niaba ya Wakuu wa Taasisi, amesemawatatekeleza maagizo yote yaliyotolewa huku akiahidi kutoa elimu kwa wananchi kuhusu kilichoandikwa katika mikataba hiyo ili wananchi waweze kujua wajibu na haki zao.

Tanzania Census 2022

Mawasiliano yetu

TBA
THE CHIEF EXECUTIVE, TANZANIA BUILDINGS AGENCY (TBA), 13 MOROGORO ROAD, P.O BOX 94, 41102 VIWANDANI, DODOMA TANZANIA, EMAIL: ce@tba.go.tz Website: www.tba.go.tz
Nukushi :
Namba ya Simu : +255 733 483 437, +255 677 108 010
Barua Pepe : barua@tba.go.tz

Linki za Haraka

Linki Linganifu

  • WIZARA YA UJENZI NA UCHUKUZI
  • Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo
  • Utumishi
  • Tume ya Takwimu ya Taifa
  • Tume ya Ajira

©2025 wakala wa majengo tanzania . Haki zote zimehifadhiwa..

Imesanifiwa, Imetengenezwa na Mamlaka ya Serikali Mtandao.Inaendeshwa na Wakala ya Majengo Tanzania