• Maswali
  • Wasiliana Nasi
  • English

Jamhuri ya Muungano wa TanzaniaWakala wa Majengo Tanzania

  • kuhusu Sisi
    • Ujumbe kutoka kwa Mtendaji Mkuu
    • Sisi ni Nani
    • Dira na Dhamira
    • Tunafanya Nini
    • Mikakati
    • Mkataba wa Huduma
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Bodi ya Ushauri
    • Muundo wa Taasisi
    • Senior Management
    • Kurugenzi wa Uwezeshaji wa Huduma
    • Kurugenzi ya Ushauri
    • Kurugenzi ya Ujenzi
    • Kurugenzi ya Miliki
    • Meneja wa Mikoa
  • Nyumba
    • Nyumba za Kuuza
    • Nyumba za Kupangisha
    • Fomu ya Ununuzi wa Nyumba
    • Fomu ya ununuzi wa Nyumba
  • Miradi
    • Miradi Tunayoishikilia
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Iliyo Katika usanifu
    • Miradi Tunayotegemea kufanya
  • Machapisho
    • Machapisho
  • Kituo Cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha
  • Ununuzi
    • Mpango wa Manunuzi wa Mwaka
    • Mialiko ya zabuni
    • Orodha ya Wazabuni Walioshinda

Habari Mpya

  • PROF. MBARAWA AIPONGEZA TBA UFUNGUZI WA MAJENGO YA KISASA DAR ES SALAAM

    tokea siku 2
  • PAC YATEMBELEA MRADI WA TEMEKE KOTA

    tokea siku 3
  • KAMATI YA BUNGE YAITAKA WIZARA YA UJENZI KUISAIDIA TBA.

    tokea wiki 1
  • BODI YA USHAURI YA TBA YATEMBELEA MRADI WA UJENZI WA TEMEKE KOTA.

    tokea wiki 2

Latest Press Release

BODI YA USHAURI YA TBA YATEMBELEA MRADI WA UJENZI WA TEMEKE KOTA.

Imewekwa: Wednesday 15, March 2023

Bodi ya Ushauri ya Wakala wa Majengo Tanzania (TBA) imetembelea na kukagua maendeleo ya mradi wa ujenzi wa nyumba za makazi katika eneo la Temeke Kota jijini Dar es Salaam.

Akizungumza mara baada ya ziara hiyo Mwenyekiti wa Bodi hiyo Arch. Dkt. Ombeni Swai amesema ziara hiyo ni muendelezo wa ufuatiatiliaji wa miradi inayotekelezwa na TBA.

"Leo tumepata nafasi ya kutembelea mradi huu ikiwa ni muendelezo wa kukagua maendeleo ya miradi inayotekelezwa na TBA katika maeneo mbalimbali nchini. Ni imani yetu kuwa malengo ya mradi huu ni kutatua changamoto ya makazi kwa wakaazi mbalimbali wa jiji la Dar es salaam amesema Arch. Dkt. Swai.

Pia Arch. Dkt. Swai amesema wanatarajia kuwa utekelezaji wa mradi huo unazingatia vigezo vyote ikiwa ni pamoja na ubora na gharama za ujenzi.

Aidha, Arch. Dkt. Swai ameiomba Serikali kutoa fedha kwa wakati ili kufanikisha malengo ya utekelezaji wa mradi huo kwa wakati.

Akiongelea miaka miwili ya Mhe. Rais Dkt.Samia Suluhu Hassan madarakani,

Arch. Dkt. Swai amesema TBA imefanikiwa kutekeleza miradi mingi ya ujenzi ikiwa ni pamoja na utekelezaji wa miradi ya ujenzi wa nyumba za Makazi kwa watumishi wa Umma katika maeneo ya Magomeni Kota, Canadian Masaki na eneo hili la Temeke Kota jijini Dar es Salaam.

Kwa upande wake Mtendaji Mkuu wa TBA Arch. Daud Kondoro amesema ziara hiyo ni muhimu kwa TBA kwakuwa inatoa fursa kupokea maoni na ushauri juu ya utekelezaji wa mradi huo ambao unatarajiwa kuchukua idadi kubwa ya Wakaazi.

Bodi ya Ushauri ya TBA imefanya ziara katika mradi wa ujenzi wa Nyumba za Makaazi katika eneo la Temeke Kota ambapo mradi huo unatekelezwa na TBA kama Mkandarasi na Mshauri Elekezi.

Tanzania Census 2022

Mawasiliano yetu

TBA
THE CHIEF EXECUTIVE, TANZANIA BUILDINGS AGENCY (TBA), 13 MOROGORO ROAD, P.O BOX 94, 41102 VIWANDANI, DODOMA TANZANIA, EMAIL: ce@tba.go.tz Website: www.tba.go.tz
Nukushi :
Namba ya Simu : +255 733 483 437, +255 677 108 010
Barua Pepe : barua@tba.go.tz

Linki za Haraka

Linki Linganifu

  • WIZARA YA UJENZI NA UCHUKUZI
  • Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo
  • Utumishi
  • Tume ya Takwimu ya Taifa
  • Tume ya Ajira

©2023 wakala wa majengo tanzania . Haki zote zimehifadhiwa..

Imesanifiwa, Imetengenezwa na Mamlaka ya Serikali Mtandao.Inaendeshwa na Wakala ya Majengo Tanzania