• Maswali
  • Wasiliana Nasi
  • English

Jamhuri ya Muungano wa TanzaniaWakala wa Majengo Tanzania

  • kuhusu Sisi
    • Ujumbe kutoka kwa Mtendaji Mkuu
    • Sisi ni Nani
    • Dira na Dhamira
    • Tunafanya Nini
    • Mikakati
    • Mkataba wa Huduma
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Bodi ya Ushauri
    • Muundo wa Taasisi
    • Senior Management
    • Kurugenzi wa Uwezeshaji wa Huduma
    • Kurugenzi ya Ushauri
    • Kurugenzi ya Ujenzi
    • Kurugenzi ya Miliki
    • Meneja wa Mikoa
  • Nyumba
    • Nyumba za Kuuza
    • Nyumba za Kupangisha
    • Fomu ya Ununuzi wa Nyumba
    • Fomu ya ununuzi wa Nyumba
  • Miradi
    • Miradi Tunayoishikilia
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Iliyo Katika usanifu
    • Miradi Tunayotegemea kufanya
  • Machapisho
    • Machapisho
  • Kituo Cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha
  • Ununuzi
    • Mpango wa Manunuzi wa Mwaka
    • Mialiko ya zabuni
    • Orodha ya Wazabuni Walioshinda

Habari Mpya

  • SERIKALI YAFUNGUA MILANGO YA UWEKEZAJI KWENYE UJENZI WA NYUMBA ZA MAKAZI

    tokea siku 3
  • MENEJIMENTI YA TBA YAHIMIZWA KUKUTANA MARA KWA MARA.

    tokea wiki 3
  • TBA YAKUTANA NA WAWEKEZAJI KUTOKA JAPAN.

    tokea wiki 3
  • TBA NA ZBA KUENDELEZA MASHIRIKIANO

    tokea wiki 3

Latest Press Release

TBA kukamilisha Mradi wa Magomeni Kota

Imewekwa: Wednesday 17, April 2019

Wakala wa Majengo Tanzania (TBA), imenunua Mitambo ya kuchakata zege pamoja na Mashine za kutengeneza tofali ambazo zitatumika kupunguza gharama za ujenzi katika miradi mbalimbali inayotekelezwa na TBA ukiwemo Mradi wa nyumba za makazi Magomeni Kota.

Hayo yamesemwa na Mhandisi Mkuu wa TBA, Jasper B. Lugemarila, aliyemwakilisha Kaimu Mtendaji Mkuu wa TBA, wakati wa ziara ya Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano anayesimamia Sekta ya Ujenzi, Mhe. Elias John Kwandikwa, alipofanya ziara ya kukagua Maendeleo ya Mradi wa Makazi wa Magomeni Kota, Aprili 13, 2019

Katika ziara hiyo, ilielezwa kuwa changamoto kubwa iliyosababisha kutokamilika kwa mradi huo kwa wakati ni mfumuko wa bei za malighafi ambazo kwa sasa zimepatiwa ufumbuzi kwa baadhi kuanza kuzalishwa na TBA wenyewe.

Mhandisi Lugemarila, alimhakikishia Mhe. Naibu Waziri kuwa wameshaandaa mpango kazi ambao utafuatwa kikamilifu ili waweze kukamilisha ujenzi huo kufikia mwishoni mwa mwaka huu.

Baada ya kukagua Maendeleo ya Ujenzi huo, Naibu Waziri Kwandikwa, alisisitiza kutoa ushirikiano kwa TBA ili waweze kukamilisha ujenzi wa Mradi huo kwa wakati kulingana na Mkakati huo mpya uliyoandaliwa.

Ujenzi wa nyumba za Magomeni Kota ukikamilika, utachangia kwa kiasi kikubwa kutatua changamoto ya makazi kwa familia 656, zikijumuisha familia 544 zilizokuwa zikiishi katika eneo hilo hapo awali.

Tanzania Census 2022

Mawasiliano yetu

TBA
THE CHIEF EXECUTIVE, TANZANIA BUILDINGS AGENCY (TBA), 13 MOROGORO ROAD, P.O BOX 94, 41102 VIWANDANI, DODOMA TANZANIA, EMAIL: ce@tba.go.tz Website: www.tba.go.tz
Nukushi :
Namba ya Simu : +255 733 483 437, +255 677 108 010
Barua Pepe : barua@tba.go.tz

Linki za Haraka

Linki Linganifu

  • WIZARA YA UJENZI NA UCHUKUZI
  • Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo
  • Utumishi
  • Tume ya Takwimu ya Taifa
  • Tume ya Ajira

©2025 wakala wa majengo tanzania . Haki zote zimehifadhiwa..

Imesanifiwa, Imetengenezwa na Mamlaka ya Serikali Mtandao.Inaendeshwa na Wakala ya Majengo Tanzania