• Maswali
  • Wasiliana Nasi
  • English

Jamhuri ya Muungano wa TanzaniaWakala wa Majengo Tanzania

  • kuhusu Sisi
    • Ujumbe kutoka kwa Mtendaji Mkuu
    • Sisi ni Nani
    • Dira na Dhamira
    • Tunafanya Nini
    • Mikakati
    • Mkataba wa Huduma
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Bodi ya Ushauri
    • Muundo wa Taasisi
    • Senior Management
    • Kurugenzi wa Uwezeshaji wa Huduma
    • Kurugenzi ya Ushauri
    • Kurugenzi ya Ujenzi
    • Kurugenzi ya Miliki
    • Meneja wa Mikoa
  • Nyumba
    • Nyumba za Kuuza
    • Nyumba za Kupangisha
    • Fomu ya Ununuzi wa Nyumba
    • Fomu ya ununuzi wa Nyumba
  • Miradi
    • Miradi Tunayoishikilia
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Iliyo Katika usanifu
    • Miradi Tunayotegemea kufanya
  • Machapisho
    • Machapisho
  • Kituo Cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha
  • Ununuzi
    • Mpango wa Manunuzi wa Mwaka
    • Mialiko ya zabuni
    • Orodha ya Wazabuni Walioshinda

Habari Mpya

  • SERIKALI YAFUNGUA MILANGO YA UWEKEZAJI KWENYE UJENZI WA NYUMBA ZA MAKAZI

    tokea mwezi 1
  • MENEJIMENTI YA TBA YAHIMIZWA KUKUTANA MARA KWA MARA.

    tokea miezi 2
  • TBA YAKUTANA NA WAWEKEZAJI KUTOKA JAPAN.

    tokea miezi 2
  • TBA NA ZBA KUENDELEZA MASHIRIKIANO

    tokea miezi 2

Latest Press Release

TBA KUSIMAMIA UKARABATI WA UWANJA WA UHURU

Imewekwa: Thursday 25, April 2024

Wakala wa Majengo Tanzania (TBA) utasimamia ukarabati wa uwanja wa Uhuru jijini Dar es Salaam ambao utafanywa na Mkandarasi CRCEG kutoka China. Hatua hiyo imekuja baada ya Kampuni hiyo kuingia Mkataba na Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo Aprili 25, 2024.

Akizungumza wakati wa utiaji saini wa mkataba huo Katibu Mkuu Wizara ya Utamaduni, Sanaa na Michezo Bw. Gerson Msigwa amesema nchi yetu imepata fursa ya kuwa mwenyeji wa mashindano makubwa ya AFCON pamoja na Kenya na Uganda ambapo kwa upande wa Tanzania tunaendelea na ujenzi na ukarabati wa viwanja vyetu ili kuweza kujiandaa kikamilifu na mashindano hayo.

Aidha, Msigwa amesema kwa hatua hiyo leo tumeshuhudia utiaji saini mkataba wa ukarabati mkubwa wa uwanja wa Uhuru ambapo zoezi zima la ukarabati litachukua kipindi cha miezi kumi na mbili (12).

Vile vile Msigwa amezipongeza TBA na Kampuni ya CRCGE kwa kuingia mkataba na Wizara kwa ajili ya ukarabati wa uwanja huo.

Awali akizungumza Naibu Katibu Mkuu wa Wizara hiyo Dkt. Suleiman Serera amesema kuwa ukarabati huo utagharimu fedha kiasi cha bilioni 19.7 ambapo ukarabati huo utajumuisha ukarabati wa miundombinu ya eneo la kuchezea (pitch), eneo la kukaa watu, mifumo ya maji safi na maji taka, viyoyozi, sauti pamoja na kubadili milango na madirisha.

Naye Kaimu Mkurugenzi wa Ushauri wa TBA Arch. Victor Balthazar amesema timu ya wataalamu kutoka TBA imejipanga kuhakikisha inasimamia ukarabati wote utakaokwenda kufanyika sambamba na kuzingatia mapendekezo yaliyotolewa na Serikali juu ya kuongeza idadi ya watu kufikia elfu thelathini.

Wakala wa Majengo Tanzania (TBA) iliingia Mkataba na Wizara ya Sanaa, Utamaduni na Michezo Februari 2023 kwa ajili ya kusimamia ukarabati wa viwanja saba nchini vikiwepo viwanja vya Uhuru na Benjamini Mkapa vilivyopo jijini Dar es Salaam.

Tanzania Census 2022

Mawasiliano yetu

TBA
THE CHIEF EXECUTIVE, TANZANIA BUILDINGS AGENCY (TBA), 13 MOROGORO ROAD, P.O BOX 94, 41102 VIWANDANI, DODOMA TANZANIA, EMAIL: ce@tba.go.tz Website: www.tba.go.tz
Nukushi :
Namba ya Simu : +255 733 483 437, +255 677 108 010
Barua Pepe : barua@tba.go.tz

Linki za Haraka

Linki Linganifu

  • WIZARA YA UJENZI NA UCHUKUZI
  • Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo
  • Utumishi
  • Tume ya Takwimu ya Taifa
  • Tume ya Ajira

©2025 wakala wa majengo tanzania . Haki zote zimehifadhiwa..

Imesanifiwa, Imetengenezwa na Mamlaka ya Serikali Mtandao.Inaendeshwa na Wakala ya Majengo Tanzania