• Maswali
  • Wasiliana Nasi
  • English

Jamhuri ya Muungano wa TanzaniaWakala wa Majengo Tanzania

  • kuhusu Sisi
    • Ujumbe kutoka kwa Mtendaji Mkuu
    • Sisi ni Nani
    • Dira na Dhamira
    • Tunafanya Nini
    • Mikakati
    • Mkataba wa Huduma
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Bodi ya Ushauri
    • Muundo wa Taasisi
    • Senior Management
    • Kurugenzi wa Uwezeshaji wa Huduma
    • Kurugenzi ya Ushauri
    • Kurugenzi ya Ujenzi
    • Kurugenzi ya Miliki
    • Meneja wa Mikoa
  • Nyumba
    • Nyumba za Kuuza
    • Nyumba za Kupangisha
    • Fomu ya Ununuzi wa Nyumba
    • Fomu ya ununuzi wa Nyumba
  • Miradi
    • Miradi Tunayoishikilia
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Iliyo Katika usanifu
    • Miradi Tunayotegemea kufanya
  • Machapisho
    • Machapisho
  • Kituo Cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha
  • Ununuzi
    • Mpango wa Manunuzi wa Mwaka
    • Mialiko ya zabuni
    • Orodha ya Wazabuni Walioshinda

Habari Mpya

  • SERIKALI YAFUNGUA MILANGO YA UWEKEZAJI KWENYE UJENZI WA NYUMBA ZA MAKAZI

    tokea mwezi 1
  • MENEJIMENTI YA TBA YAHIMIZWA KUKUTANA MARA KWA MARA.

    tokea miezi 2
  • TBA YAKUTANA NA WAWEKEZAJI KUTOKA JAPAN.

    tokea miezi 2
  • TBA NA ZBA KUENDELEZA MASHIRIKIANO

    tokea miezi 2

Latest Press Release

?TBA YAPONGEZWA KWA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAENDELEO MKOANI TABORA

Imewekwa: Thursday 09, April 2020

TBA YAPONGEZWA KWA UTEKELEZAJI WA MIRADI YA MAENDELEO MKOANI TABORA

Wakala wa Majengo Tanzania (TBA) wapongezwa kwa kuendelea kutekeleza miradi ya maendeleo Mkoani Tabora. Uongozi wa Mkoa wa Tabora ulitoa jukumu kwa TBA kusimamia na kujenga miradi ya maendeleo kwa ubora na viwango vinavyohitajika katika majengo mbalimbali mkoani humo.

Hatua ya kuipongeza TBA Mkoani Tabora imekuja baada ya Katibu Tawala Wilaya ya Kaliua Bw. Michael Nyahinga kujiridhisha na hatua ya utekelezaji wa miradi ya ujenzi wa nyumba za viongozi katika Wilaya ya Kaliua. Bw. Nyahinga alisema TBA imefanya kazi kubwa na nzuri ambayo inastahili pongezi kwani nyumba hizo zina ubora na zimejengwa kwa wakati ndani ya mkataba.

Kaimu Meneja wa TBA Mkoa wa Tabora Mhandisi Abraham Ndazi amesema TBA inatekeleza miradi ya aina tatu ambayo ni Ubunifu na Ujenzi, Ushauri pamoja na ukarabati. Miradi ya Ubunifu na Ujenzi inayotekelezwa Mkoani Tabora ni pamoja na ujenzi wa Nyumba ya makazi ya Katibu Tawala wa Tabora mjini, Nyumba ya makazi ya Mkuu wa Wilaya na Katibu Tawala Wilaya ya Kaliua pamoja na Nyumba za makazi za Maafisa Waandamizi Wilaya ya Kaliua. Pia katika miradi ya Ushauri inayotekelezwa ni pamoja na Ujenzi wa jengo la ofisi ya Halmashauri ya Wilaya ya Nzega, Ukarabati wa jengo la Ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Tabora na Ujenzi wa jengo la Utumishi wa Umma Mkoani Tabora.

Aidha, Mhandisi Abraham Ndazi alisema mafanikio ya utekelezaji wa miradi hiyo ya maendeleo Mkoani Tabora yanatokana na ushirikiano mzuri unaotolewa na washitiri kwa TBA. Vile vile Mhandisi Ndazi ameongeza kuwa ofisi yake ina mkakati wa kukarabati karakana kwa lengo la kuzalisha samani ambazo zitakuwa na ubora na kuongeza mapato kwa TBA.

Wakala wa Majengo Tanzania (TBA) ni taasisi ya Serikali iliyoanzishwa mwaka 2002 kwa lengo la kusimamia miliki za Serikali.

Tanzania Census 2022

Mawasiliano yetu

TBA
THE CHIEF EXECUTIVE, TANZANIA BUILDINGS AGENCY (TBA), 13 MOROGORO ROAD, P.O BOX 94, 41102 VIWANDANI, DODOMA TANZANIA, EMAIL: ce@tba.go.tz Website: www.tba.go.tz
Nukushi :
Namba ya Simu : +255 733 483 437, +255 677 108 010
Barua Pepe : barua@tba.go.tz

Linki za Haraka

Linki Linganifu

  • WIZARA YA UJENZI NA UCHUKUZI
  • Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo
  • Utumishi
  • Tume ya Takwimu ya Taifa
  • Tume ya Ajira

©2025 wakala wa majengo tanzania . Haki zote zimehifadhiwa..

Imesanifiwa, Imetengenezwa na Mamlaka ya Serikali Mtandao.Inaendeshwa na Wakala ya Majengo Tanzania