• Maswali
  • Wasiliana Nasi
  • English

Jamhuri ya Muungano wa TanzaniaWakala wa Majengo Tanzania

  • kuhusu Sisi
    • Ujumbe kutoka kwa Mtendaji Mkuu
    • Sisi ni Nani
    • Dira na Dhamira
    • Tunafanya Nini
    • Mikakati
    • Mkataba wa Huduma
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Bodi ya Ushauri
    • Muundo wa Taasisi
    • Senior Management
    • Kurugenzi wa Uwezeshaji wa Huduma
    • Kurugenzi ya Ushauri
    • Kurugenzi ya Ujenzi
    • Kurugenzi ya Miliki
    • Meneja wa Mikoa
  • Nyumba
    • Nyumba za Kuuza
    • Nyumba za Kupangisha
    • Fomu ya Ununuzi wa Nyumba
    • Fomu ya ununuzi wa Nyumba
  • Miradi
    • Miradi Tunayoishikilia
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Iliyo Katika usanifu
    • Miradi Tunayotegemea kufanya
  • Machapisho
    • Machapisho
  • Kituo Cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha
  • Ununuzi
    • Mpango wa Manunuzi wa Mwaka
    • Mialiko ya zabuni
    • Orodha ya Wazabuni Walioshinda

Habari Mpya

  • SERIKALI YAFUNGUA MILANGO YA UWEKEZAJI KWENYE UJENZI WA NYUMBA ZA MAKAZI

    tokea mwezi 1
  • MENEJIMENTI YA TBA YAHIMIZWA KUKUTANA MARA KWA MARA.

    tokea miezi 2
  • TBA YAKUTANA NA WAWEKEZAJI KUTOKA JAPAN.

    tokea miezi 2
  • TBA NA ZBA KUENDELEZA MASHIRIKIANO

    tokea miezi 2

Latest Press Release

TBA YASHIRIKI UJENZI WA KITUO CHA PAMOJA CHA FORODHA KASUMULU

Imewekwa: Wednesday 25, March 2020

TBA YASHIRIKI UJENZI WA KITUO CHA PAMOJA CHA FORODHA KASUMULU

Wakala wa Majengo Tanzania (TBA) unashiriki kama Mshauri Elekezi Msaidizi (Sub-Consultant) katika utekelezaji wa mradi wa Ujenzi wa Kituo cha Pamoja cha Forodha mpakani mwa Tanzania na Malawi unaoendelea katika eneo la Kasumulu, Mkoani Mbeya. Mradi huu unatarajiwa kuwa na faida kubwa katika kukuza ushirikiano baina ya nchi hizi mbili pamoja na kuchochea fursa za kibiashara kati ya Tanzania na Malawi. Mradi huu utakapokamilika utarahisisha usafirishaji wa watu na mizigo kutoka pande zote mbili hivyo kuchochea ukuaji wa biashara pamoja na uchumi kwa ujumla.

Akielezea juu utekelezaji wa mradi huu, Arch. Daniel Mandari amesema utekelezaji wa mradi unaendelea vizuri kwa kuzingatia viwango vya ubora unaotakiwa. Pia amesema mradi huu ni muhimu kwa wananchi na taifa kwa ujumla kwa kuwa utakuza wigo wa bishara kati ya Tanzania na Malawi.

Arch. Mandari aliongeza kuwa katika mradi huu, TBA kama Mshauri Elekezi Msaidizi (Sub-Consultant) inashirikiana vizuri na kampuni ya CGC kutoka China ambayo ndiyo mkandarasi na kampuni ya EGC kutoka Misri ambayo ndiyo Mshauri Elekezi. Pia alieleza kuwa mradi huu unakabiliwa na changamoto ya mvua ambayo kwa kiasi fulani inaathiri kasi ya utekelezaji wa mradi kwa sababu kazi za ujenzi wa barabara zinaathirika sana na uwepo wa mvua zinazoendelea kunyesha nchini.

Kwa upande wa Meneja mradi kutoka kampuni ya CGC, Mhandisi Zhao amesema katika kutekeleza mradi huu huwa wanajadiliana na wataalam wa TBA kwa kila hatua ya utekelezaji wa mradi na wakikubaliana wanaendelea na kazi. Aliongeza kwa kusema kuwa wataalam wa TBA wana uzoefu mkubwa na kunapokuwa na mashaka na kitu wanapata nafasi ya kuwauliza na kupokea mapendekezo yanayowawezesha kufanya kazi nzuri na kwa viwango vinavyohitajika.

Imetolewa na Kitengo cha Mawasiliano kwa Umma na Masoko – TBA

25 Machi, 2020


Tanzania Census 2022

Mawasiliano yetu

TBA
THE CHIEF EXECUTIVE, TANZANIA BUILDINGS AGENCY (TBA), 13 MOROGORO ROAD, P.O BOX 94, 41102 VIWANDANI, DODOMA TANZANIA, EMAIL: ce@tba.go.tz Website: www.tba.go.tz
Nukushi :
Namba ya Simu : +255 733 483 437, +255 677 108 010
Barua Pepe : barua@tba.go.tz

Linki za Haraka

Linki Linganifu

  • WIZARA YA UJENZI NA UCHUKUZI
  • Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo
  • Utumishi
  • Tume ya Takwimu ya Taifa
  • Tume ya Ajira

©2025 wakala wa majengo tanzania . Haki zote zimehifadhiwa..

Imesanifiwa, Imetengenezwa na Mamlaka ya Serikali Mtandao.Inaendeshwa na Wakala ya Majengo Tanzania