• Maswali
  • Wasiliana Nasi
  • English

Jamhuri ya Muungano wa TanzaniaWakala wa Majengo Tanzania

  • kuhusu Sisi
    • Ujumbe kutoka kwa Mtendaji Mkuu
    • Sisi ni Nani
    • Dira na Dhamira
    • Tunafanya Nini
    • Mikakati
    • Mkataba wa Huduma
  • Utawala
    • Muundo wa Taasisi
    • Bodi ya Ushauri
    • Muundo wa Taasisi
    • Senior Management
    • Kurugenzi wa Uwezeshaji wa Huduma
    • Kurugenzi ya Ushauri
    • Kurugenzi ya Ujenzi
    • Kurugenzi ya Miliki
    • Meneja wa Mikoa
  • Nyumba
    • Nyumba za Kuuza
    • Nyumba za Kupangisha
    • Fomu ya Ununuzi wa Nyumba
    • Fomu ya ununuzi wa Nyumba
  • Miradi
    • Miradi Tunayoishikilia
    • Miradi Inayoendelea
    • Miradi Iliyokamilika
    • Miradi Iliyo Katika usanifu
    • Miradi Tunayotegemea kufanya
  • Machapisho
    • Machapisho
  • Kituo Cha Habari
    • Taarifa kwa vyombo vya habari
    • Hotuba
    • Maktaba ya Video
    • Maktaba ya Picha
  • Ununuzi
    • Mpango wa Manunuzi wa Mwaka
    • Mialiko ya zabuni
    • Orodha ya Wazabuni Walioshinda

Habari Mpya

  • SERIKALI YAFUNGUA MILANGO YA UWEKEZAJI KWENYE UJENZI WA NYUMBA ZA MAKAZI

    tokea mwezi 1
  • MENEJIMENTI YA TBA YAHIMIZWA KUKUTANA MARA KWA MARA.

    tokea miezi 2
  • TBA YAKUTANA NA WAWEKEZAJI KUTOKA JAPAN.

    tokea miezi 2
  • TBA NA ZBA KUENDELEZA MASHIRIKIANO

    tokea miezi 2

Latest Press Release

UONGOZI WA MKOA WA SONGWE WARIDHISHWA NA KASI YA UTEKELEZAJI WA MIRADI INAYOTEKELEZWA NA TBA

Imewekwa: Monday 23, March 2020

UONGOZI WA MKOA WA SONGWE WARIDHISHWA NA KASI YA UTEKELEZAJI WA MIRADI INAYOTEKELEZWA NA TBA

Uongozi wa Mkoa wa Songwe umeridhishwa na kasi ya utekelezaji wa miradi inayotekelezwa na TBA mkoani humo. Hayo yameelezwa na Katibu Tawala wa Mkoa wa Songwe Mhe. David Kafulila na Bi. Regina Bieda Mkurugenzi wa Halmashauri ya Mji wa Tunduma. Mhe. Kafulila ameitaja miradi hiyo kuwa ni ujenzi wa jengo la ofisi ya Mkuu wa Mkoa wa Songwe linalojengwa eneo la Mselewa Wilayani Mbozi, ujenzi wa jengo la Hospitali ya Wilaya ya Tunduma, pamoja na ujenzi wa jengo la ofisi ya Mkurugenzi Mtendaji Halmashauri ya Wilaya ya Songwe.

Mhe. Kafulila amesema kasi ya utekelezaji wa miradi hiyo ni kubwa kinyume na matarajio ya ofisi yake na amethibitisha kuwa TBA inafanya kazi nzuri sana mkoani Songwe achilia mbali changamoto kadhaa zilizojitokeza hasa suala la fedha kutoka katika ofisi yake ya Mkoa.

Vile vile Mhe. Kafulila amepongeza jitihada na ushirikiano mkubwa unaotolewa na TBA mkoani Songwe katika kusukuma kasi ya utekekelezaji wa miradi ya maendeleo inayotekelezwa katika Mkoa huo.

Aidha, Mkurugenzi Mtendaji wa Halmashauri ya Mji wa Tunduma Bi. Regina Bieda amesema anatambua jitihada zinazoendelea kufanywa na TBA Mkoa wa Songwe kuwa zimezaa matunda hasa katika kuharakisha utekelezaji wa miradi hiyo mikubwa ya maendeleo. Pia, amepongeza utendaji mzuri na ushirikiano mkubwa wa TBA Mkoa wa Songwe na kuonesha nia ya kuendelea kufanya kazi na Wakala wa Majengo Tanzania (TBA).

Naye Kaimu Meneja wa TBA Mkoa wa Songwe Arch. Steven Simba amesema, ofisi yake inajukumu kubwa la kuendelea kutekeleza kwa wakati miradi yote iliyochini ya TBA katika Mkoa wa Songwe kwa kuzingatia ubora, muda wa mkataba na gharama nafuu

Tanzania Census 2022

Mawasiliano yetu

TBA
THE CHIEF EXECUTIVE, TANZANIA BUILDINGS AGENCY (TBA), 13 MOROGORO ROAD, P.O BOX 94, 41102 VIWANDANI, DODOMA TANZANIA, EMAIL: ce@tba.go.tz Website: www.tba.go.tz
Nukushi :
Namba ya Simu : +255 733 483 437, +255 677 108 010
Barua Pepe : barua@tba.go.tz

Linki za Haraka

Linki Linganifu

  • WIZARA YA UJENZI NA UCHUKUZI
  • Wizara ya Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo
  • Utumishi
  • Tume ya Takwimu ya Taifa
  • Tume ya Ajira

©2025 wakala wa majengo tanzania . Haki zote zimehifadhiwa..

Imesanifiwa, Imetengenezwa na Mamlaka ya Serikali Mtandao.Inaendeshwa na Wakala ya Majengo Tanzania